Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Lokua Kanza, balozi wa kitaifa wa UNICEF nchini DRC kuhusu elimu ametembelea shule aliyosoma utotoni na kusihi wanafunzi kuzingatia umuhimu wa elimu
UNICEF/Josue Mulala

Mwanamuziki Lokua Kanza atoa ujumbe kwa wanafunzi nchini DRC

Lokua Kanza, mwanamuziki nguli ndani  na nje ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni balozi wa kitaifa wa elimu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo, ametumia ziara yake katika shule ya msingi aliyosoma utotoni ili kuchagiza wanafunzi wa kike na wa kiume kupatia kipaumbele suala la elimu. 

 

Sauti
2'22"
"Shujaa wangu ni wewe," ni kitabu kipya kilichozinduliwa leo kusaidia watoto kuelewa kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19
WHO

WHO na UNICEF wazindua kitabu cha watoto kuhusu COVID-19

Kitabu kipya kilichopewa jina “Shujaa Wangu ni Wewe 2021” au “My Hero is You 2021” ambacho kimezinduliwa mwishoni mwa wiki na mashirika ya kibinadamu yakiwemo ya Umoja wa Mataifa kina lengo la kuwapa Watoto matumaini ya kuendelea na maisha hasa wakati huu wa janga la corona au COVID-19 limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na lile la kuhudumia Watoto la UNICEF. 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Peter Mathuki (kulia) akihojiwa na Leah Mushi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kando mwa Mjadala Mkuu wa UNGA76
UN News/Assumpta Massoi

Hatma ya DRC kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mikononi mwa Mawaziri wa jumuiya hiyo

Wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa nchi duniani kuimarisha ushirikiano wa kimataifa iwe kikanda au kidunia unazidi kuitikiwa ambapo Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC inachukua hatua kupanua wigo wa uanachama wake kutoka 6 hadi 7 kwa kufanya kikao cha kujadili ombi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kujiunga na chombo hicho. 

 

Sauti
2'9"
Rais wa UNGA76 Abdullah Shahid akifunga mjadala mkuu wa UNGA76 jijini New York, Marekani 27 Septemba 2021
UN/Cia Pak

Rais wa UNGA76 afunga pazia la mjadala mkuu; asema ushirikiano wa kimataifa ungali hai

Hatimaye mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 umefunga pazia leo Jumatatu katika makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani huku Rais wa Baraza hilo Abdullah Shahid akisema mkutano huo umefanyika kwa mafaniko makubwa katikati ya janga la Corona au COVID-19 huku akitaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni hatua bora za kupunguza maambukizi na viwango vya juu vya chanjo.