Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katika kituo cha ukusanyaji wa pamba Brazil ambako pamba hutenganishwa na mbegu kabla haijashindiliwa na kuhifadhiwa
FAO/Alberto Conti

Pamba, kitambaa kinachositiri  zaidi ya familia milioni 100 duniani:UN

 Leo ni siku ya pamba duniani ikiwa ni maadhimisho ya kwanza kabisa ya siku hiyo kuenzi zao ambalo kitabaa chake kinatengeneza mavazi ya kila siku yaliyosheheni kwenye mkabati mengi ya nguo na ni kitambaa kizuri, rahisi kuvaa, kukitunza na kinadumu kwa muda mrefu. Lakini kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa thamani ya pamba ni zaidi ya kitambaa kama inavyofafanua taarifa ya Flora Nducha 

Sauti
2'40"
Rais wa UNGA76 Abdullah Shahid akifunga mjadala mkuu wa UNGA76 jijini New York, Marekani 27 Septemba 2021
UN/Cia Pak

Rais wa UNGA76 afunga pazia la mjadala mkuu; asema ushirikiano wa kimataifa ungali hai

Hatimaye mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 umefunga pazia leo Jumatatu katika makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani huku Rais wa Baraza hilo Abdullah Shahid akisema mkutano huo umefanyika kwa mafaniko makubwa katikati ya janga la Corona au COVID-19 huku akitaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni hatua bora za kupunguza maambukizi na viwango vya juu vya chanjo.

 

Dr.Alinda Mashiku

Penye nia pana njia kama nimefika NASA nawe utaweza: Mhandisi Dkt.Alinda Mashiku 

Mwanamke Mtanzania angara kituo cha safari za anga cha Marekani NASA  tawi la Goddard mjini Maryland lililojikita na ufuatiliaji wa safari za satellite. Dkt. Alinda Mashiku ambaye amekuwa NASA kwa miaka minane sasa anasema ilimchukua miaka 12 hadi kuajiriwa NASA kama mhandisi na sasa pia ni meneja wa kitengo cha kuhakikisha satellite zonazokwenda angani hazigongani. Je anahisi vipi kuwa miongoni mwa wanawake wachache wahandisi NASA na safari yake ilianza vipi? Kufahamu yote hayo na mengine mengi ungana na Flora Nducha wa UN News Kiswahili aliyeketi na kuzungumza naye katika makala hii  

Sauti
13'39"
Vijana hawa wa kikundi cha kuweka na kukopa cha Kyambogho II wilayani Kasese nchini Uganda wakijifunza stadi za uoakaji kama sehemu ya kujikwamua na COVID-19.
© UNICEF/Henry Bongyereirwe

Mradi wa Uganda Yield Fund wawasaidia wajasiriamali Uganda wakati wa COVID-19  

Uganda Yield Fund ambao ni ufadhili kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD ikishirikiana na Muungano wa Ulaya, UE, na serikali ya Uganda, umeisaidia sekta binafsi nchini Uganda ambayo nayo imewezesha wajasiriamali wadogowadogo ili wasiathiriwe sana na hivyo kuwa na mnepo  hata katika mazingira ya Covid-19.