Virusi vya Corona sasa vyatangazwa kuwa dharura ya kiafya ya kimataifa
Mkutano wa pili wa kamati ya dharura ulioitishwa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la afya duniani, WHO, chini ya sheria za kimataifa za afya (IHR) (2015) kuhusiana na mlipuko wa virusi vya corona 2019-nCoV nchini China, umeutangaza mlipuko huowa virusi vya corona kuwa ni dharura ya kiafya ya kimataifa, PHEIC.