Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Abiria wakiwa wamejikinga na maambukizi ya mfumo wa hewa wakiwa katika treni za chini ya ardhi huko Shenzhen China
UN News/Jing Zhang

Virusi vya Corona sasa vyatangazwa kuwa dharura ya kiafya ya kimataifa

Mkutano wa pili wa kamati ya dharura ulioitishwa hii leo mjini Geneva Uswisi na shirika la afya duniani, WHO, chini ya sheria za kimataifa za afya (IHR) (2015) kuhusiana na mlipuko wa virusi vya corona 2019-nCoV nchini China, umeutangaza mlipuko huowa virusi vya corona kuwa ni dharura ya kiafya ya kimataifa, PHEIC.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres ahudhuria Maadhimisho ya Makumbusho ya Kumi ya mtetemeko ya ardhi ya Haiti ya tarehe 12 Januari 2010
UN Photo/Evan Schneider

Waathirikwa wa tetemeko la miaka 10 iliyopita Haiti waenziwa na UN

Zaidi ya watu 200,000 waliopoteza maisha wakati tetemeko kubwa lilipokikumba kisiwa cha Haiti miaka 10 iliyopita leo wameenziwa katika sherehe maalum ya kumbukumbu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New york ikijumuisha pia wafanyakazi 102 wa Umoja wa Mataifa waliopoteza maisha pia ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya wafanyakazi kufa katika tukio moja kwenye historia ya Umoja wa Mataifa.