Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Familia ambazo ni manusura wa kimbunga Idai , zikihamishiwa kutoka makazi ya muda huko IFAPA mjini BEIRA kwenda kituo jirani na makazi yao ya awali wilayani Buzi nchini Msumbiji.
© UNHCR/Luiz Fernando Godinho

Manusura wa IDAI wasogezwa karibu na nyumbani - UNHCR

Familia zilizonusurika na kutawanywa na kimbunga Idai nchini Msumbiji zimeanza kuhamishiwa katika maeneo yaliyo karibu na mahali walikotoka wakati wa zahma hiyo. Kwa mujibu swa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR zoezi hilo linaendeshwa kwa ushirikiano na serikali ya Msumbiji na washirika wengine .

Sauti
1'36"