Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kikao cha Kwanza cha Baraza Kuu la ushirikiano wa mataifa (sasa Umoja wa Mataifa) Hii ni tarehe 10 January mwaka 1946 huko London, Uingereza. Ni katka kikao hiki, Brazil ilikuwa mjumbe wa Baraza Kuu na lile la usalama.
UN /Marcel Bolomey

Kwanini Brazil huwa ya kwanza kuhutubia UNGA?

Kawaida ni rais wa Brazil ndiye hufungua vikao vya ngazi za juu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Lakini ni kwa nini? Utaratibu huu ulianza katika kikao cha mwanzo kabisa kilichofanyika mjini London, Uingereza Januari 10 mwaka 1946. Tangu wakati huo Brazil imekuwa kila mara inakuwa ya kwanza katika ratiba za viongozi kuhutubia mjadala wa wazi wa Baraza hilo unaofanyika kila mwezi Septemba.