Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Zeid Ra'ad Al Hussein mkuu wa kamisheni ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, akitoa hotuba mjini Vienna, Austria wakati wa kuadhimisha miaka 25 ya mkutano wa dunia kuhusu haki za binadamu
Picha ya UNIS Vienna/Lilia Jiménez-Ertl

Haki za binadamu ziko mashakani kwa sasa-Zeid

Dunia inarudi nyuma katika masuala ya haki za binadamu  na misingi yake inavurugwa kila upande wa dunia hii, ameonya  Jumanne, afisa wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa,na kumhimiza kila mtu popote alipo kuonyesha  azma ya kujitolea katika kulinda haki hizo.