Haki za binadamu ziko mashakani kwa sasa-Zeid

Dunia inarudi nyuma katika masuala ya haki za binadamu na misingi yake inavurugwa kila upande wa dunia hii, ameonya Jumanne, afisa wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa,na kumhimiza kila mtu popote alipo kuonyesha azma ya kujitolea katika kulinda haki hizo.
Katika hotuba, inayoonekana kama kali kuadhimisha miaka 25 ya mkutano wa dunia kuhusu haki za binadamu ambayo ilitilia mkazo wa hali ya haki za binadamu ambazo ni za wote hazibadiliki na kuwa na uhusiano, mkuu wa tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Al Hussein, amesema kuwa baada ya robo karne kupita, ulimwengu unaonekana kama, unageuza mkondo.
Katika mkutano wa 1993, mataifa 171 yalipasisha tamko la Vienna lenye mpango tekelezi, wa kuimarisha haki za binadamu duniani kote. Hiyo ilionekana kwa wengi, kama muhimili wa haki zote za wakati wa baada ya vita baridi.
Pia mkutano huo ulianzisha mchakato wa kuunda ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, kwa kifupi OHCHR ,inayoongozwa kwa sasa na Bw Zeid mwenyewe.
Akihutubia mkutano huo Jumanne, afisa huyo wa haki za binadamu kutoka Umoja wa Mataifa, amesema kuwa kuna kurudi nyuma hadi wakati ambapo ubaguzi wa rangi pamoja na chuki dhidi ya wageni, vikichochea, kimakusudi, chuki na ubaguzi miongoni mwa umma, kwa kisingizio cha demokrasia na utawala wa sheria.
Ameonya kuwa, sanasana katika bara la Ulaya, vyama vya kisiasa vinavyoegemea sana katika misingi ya kikabila vinaongezeka kila mara katika mataifa mengi na vinachochea chuki pamoja na mgawanyiko.
Endapo vyama hivyo vikishika madaraka, kimakusidi husambaza mtazamo wa uongo kuwahusu wahamiaji pamoja na wanaharakati wanaotetea haki za binadamu.
Karibu kila mahali, Ulaya nzima, chuki dhidi ya wahamiaji imepenyeza hata katika vyama vikuu na kupoteza dira ya mwelekeo kisiasa kuelekea ghasia na mateso.
Leo si wakati wa kufumbia macho
Akibaini vitisho dhidi ya haki za binadamu duniani kote, ambavyo sasa havichukuliwi kama kipaumbele bali kuchukuliwa kama kitu cha chini sana, amemuomba kila mtu kusimama kidete kutetea kile kinachiowalisha tamko la Vienna.
“Tunahitajika kutumia maadhimisho haya kuanza kuihamasisha jamii kulinda haki za binadamu kwa dhati,” amesema Bw Zeid, huku akikariri haja ya kuweka wazi alichoita, “haki za binadamu muhimu kwa maisha ya kawaida ya mwanadamu pamoja na mustakbala wa binadamu wenzetu.”
Ameongeza kuwa “Hakuna cha kupoteza muda sasa. Acha hii iwe ndio kichocheo, ili tamko la Vienna lichomoze sio kama kitu cha mambo ya kale kinachozeeka , bali kama mshika bendera wa vuguvugu lenye nia ya kujenga amani na maendeleo” amesema.