Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jaribio la Mapinduzi Guinea-Bissau limelaaniwa na KM Ban

Kwenye risala iliotolewa, kwa kupitia msemaji wake, KM Ban Ki-moon ameshtumu vikali mashambulio ya Ijumapili dhidi ya makazi ya Raisi Bernardo Joao Vieira, yaliotukia Bissau, mji mkuu wa Guinea-Bissau yalioendelezwa na baadhi ya wanajeshi, wiki moja tu baada ya kufanyika uchaguzi wa bunge nchini humo.

Mkataba wa kupiga marufuku mabomu yaliotegwa ardhini unafanyiwa mapitio Geneva

Mjini Geneva, Uswiss kulifunguliwa rasmi, leo hii, kikao cha 9 cha Mataifa Yalioidhinisha Mkataba wa Kupiga Marufuku Mabomu Yaliotegwa Ardhini ambapo risala ya Raisi wa mkutano, Balozi Jurg Streuli ilikumbusha kwamba licha ya kuwa mabomu milioni 40 ya kutega yalifanikiwa kuangamizwa kimataifa, mapaka sasa, na wakati huo huo kilomita kadhaa za ardhi zilifufuliwa baada ya mabomu hayo kuteketezwa, hata hivyo majukumu makubwa na mazito bado yamesalia na yatakikana kufyeka silaha hizi ovu katika maeneo kadha wa kadha ya dunia.

Hapa na Pale

Ripoti ya hivi karibuni ya KM, kuhusu hali ya watoto kwenye mazingira ya mapigano yaliopamba katika JKK imethibitisha kuteremka idadi ya vitendo vilivyokiuka sana haki za watoto nchini. Ripoti ilbainisha kupatikana maendeleo machache kwenye zile juhudi za kuwapokonya watoto silaha na kuwajumuisha kimaisha kwenye jamii za kawaida. Juu ya hivyo, ripoti ilisisitiza, watoto bado wanaendelea kuwawa mwanzo kuathiriwa kwenye mgogoro wa katika Kivu Kaskazini na Kusini pamoja na Katanga Kaskazini. Kadhalika, ripoti iliendelea kusema, watoto wenye umri mdogo hulazimishwa kushiriki kwenye mapigano, na wakati huo huo wanaendelea kunajisiwa na makundi mbalimbali yenye silaha, vitendo ambavyo, ripoti ilisema, vinafanyika kwa wingi zaidi kwenye maeneo ya vurugu.

Nchi tatu zakutikana kuvunja sheria ya Mkataba Dhidi ya Mabomu ya Kutega

Ripoti ya 2008 kuhusu namna Mataifa Wanachama yanavyotekeleza yale mapendekezo ya Mkataba wa Kupiga Marufuku Matumizi ya Mabomu Yaliotegwa Ardhini, iliowakilishwa rasmi hii leo katika UM, imebainisha nchi tatu wanachama zimeharamisha kanuni za Mkataba huo, kwa kushindwa kuangamiza silaha hizo kwa wakati; mataifa yenyewe ni Ugiriki, Uturuki na Belarus.