Hapa na Pale
Baraza la Usalama lilikutana Alkhamisi asubuhi kuzungumzia hali ya amani na usalama katika bara la Afrika. Wajumbe wa Baraza walipata fursa ya kumsikiliza Raisi Ismail Omar Guelleh wa Djbouti akizungumzia kuzuka kwa hali ya wasiwasi, na mvutano hivi karibuni, baina ya taifa lake na nchi jirani ya Eritrea. Mwakilishi wa Eritrea, Araya Desta pia alihutubia Baraza la Usalama baadaye. Mkutano wa leo wa Baraza la Usalama uliadhimisha kikao cha 6,000 cha taasisi hii ya UM.~