Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na Pale

Baraza la Usalama lilikutana Alkhamisi asubuhi kuzungumzia hali ya amani na usalama katika bara la Afrika. Wajumbe wa Baraza walipata fursa ya kumsikiliza Raisi Ismail Omar Guelleh wa Djbouti akizungumzia kuzuka kwa hali ya wasiwasi, na mvutano hivi karibuni, baina ya taifa lake na nchi jirani ya Eritrea. Mwakilishi wa Eritrea, Araya Desta pia alihutubia Baraza la Usalama baadaye. Mkutano wa leo wa Baraza la Usalama uliadhimisha kikao cha 6,000 cha taasisi hii ya UM.~

WFP itafadhilia watoto Usomali msaada wa chakula dhidi ya utapiamlo

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) linatarajiwa karibuni kuanza kupeleka misaada ya chakula cha dharura chenye rutubishi kubwa katika Usomali, aina ya biskuti zilizotengenezewa njugu na karanga, ikiwa miongoni mwa juhudi za kuwakinga watoto na hatari inayoendelea kukithiri ya utapiamlo mbaya uliozuka nchini humo uliopaliliwa zaidi na mapigano.

Kemikali tatu zazingatiwa kuchungwa kimataifa

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) imeripoti kwamba kuanzia wiki ijayo maofisa wa kimataifa kutoka serikali 120 ziada watakutana mjini Roma, Utaliana kujadiliana kama aina [mbili] za kemikali zinazotumiwa hivi sasa ulimwenguni ziingizwe kwenye ile orodha inayojulikana kama Orodha ya PIC.

Jumuiya ya Muungano wa Dini za Kimataifa kubuniwa rasmi Istanbul

Mkutano ulioandaliwa na Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kudhibiti Idadi ya Watu (UNFPA) uliofanyika Istanbul, Uturuki kuzingatia mchango wa mashirika ya kidini katika kupambana na janga la UKIMWI .. na umaskini umemaliza mijadala yake ya siku mbili Ijumanne na kuafikiana kubuni jumuiya mpya itakayowakilisha dini zote kuu za ulimwengu, ikijumlisha Ukristo, Uislam, Uyahudi, pamoja na dini za Kihindu, Kibudha na Kisingasinga. Taasisi hii mpya itajulikana kwa jina la Jumuiya ya Mungano wa Dini za Kimataifa. ~

Hapa na Pale

Alkhamisi (23 Oktoba) KM Ban Ki-moon atakutana na wataalamu wa watano wa uchumi, wa madaraka ya juu kimataifa, kwa makusudio ya kutathminia taathira za fedha kwenye kazi za UM duniani, na kulenga zaidi mashauriano yao kwenye juhudi za kutekeleza Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na kukabiliana na taathira za mabadiliko ya hali ya hewa. KM alieleza, kwa kupitia msemaji wake, kwamba ni lazima kwa walimwengu kujumuika kwa moyo wa ushirikiano kukabiliana, kwa mafanaikio, na tatizo sugu la fedha kwenye soko la kimataifa, hasa ilivyokuwa mgogoro huu huumiza zaidi umma dhaifu na maskini.~