Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP itafadhilia watoto Usomali msaada wa chakula dhidi ya utapiamlo

WFP itafadhilia watoto Usomali msaada wa chakula dhidi ya utapiamlo

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) linatarajiwa karibuni kuanza kupeleka misaada ya chakula cha dharura chenye rutubishi kubwa katika Usomali, aina ya biskuti zilizotengenezewa njugu na karanga, ikiwa miongoni mwa juhudi za kuwakinga watoto na hatari inayoendelea kukithiri ya utapiamlo mbaya uliozuka nchini humo uliopaliliwa zaidi na mapigano.