Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Raisi wa BK ameanzisha tume maalumu ya kupitia mfumo wa fedha duniani

Raisi wa BK ameanzisha tume maalumu ya kupitia mfumo wa fedha duniani

Raisi wa kikao cha 63 cha Baraza Kuu la UM, Miguel d’Escoto ametangaza kuanzisha tume maalumu ya hadhi ya juu kabisa, itakayofanya mapitio juu ya mfumo wa fedha wa kimataifa kama unahitajia marekibisho, ikijumlisha pia zile taasisi za fedha za kimataifa kama Benki Kuu ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).