Hapa na Pale (Taarifa za Kusoma)
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kwamba wiki iliopita watu 12,000 waliuhajiri mji wa Mogadishu, Usomali kwa sababu ya mapigano makali yaliozuka baina ya wapiganaji wafuasi wa makundi ya KiIslam, wenye kupinga serikali, dhidi ya na vikosi vya serikali vinavyoungwa mkono na majeshi ya Ethiopia yaliopo nchini. Nusu ya wahamiaji waliong’olewa makwao walipatiwa makazi ya muda karibu na mji, na nusu nyengine walikimbilia mji wa Afgooye ,uliopo kilomita 3o kusini-magharibi ya Mogadishu.