Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakulima wadogo wadogo wanazingatiwa misaada ya kujitegemea

Wakulima wadogo wadogo wanazingatiwa misaada ya kujitegemea

Hapa Makao Makuu leo asubuhi kulifanyika warsha kadha wa kadha juu ya masuala yanayohusu juhudi za kukuza maendeleo katika nchi maskini. Kwenye mkusanyiko mmoja kuliwasilishwa mradi mpya utakaofadhiliwa na wakf za kimataifa na kuwasaidia wakulima wadogo wadogo kukuza pato na kujitegemea kimaisha.