Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUC yaripoti "utulivu dhaifu" warejea Kivu Kaskazini

MONUC yaripoti "utulivu dhaifu" warejea Kivu Kaskazini

Shirika la UM la Ulinzi wa Amani katika JKK (MONUC) limeripoti “utulivu dhaifu” umerejea katika jimbo la Kivu Kaskazini, hususan kwenye mji wa Sake, ambapo karibuni kulitukia mapigano makali kati ya vikosi vya Serikali (FARDC) na wafuasi wa kundi la waasi la CNDP.