Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DPRK imeamua kuanzisha shughuli za viwanda vya nyuklia Yongbyon

DPRK imeamua kuanzisha shughuli za viwanda vya nyuklia Yongbyon

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) yaani Mohamed ElBaradei aliripoti Ijumatatu kwamba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Umma wa Korea (DPRK) au Korea ya Kaskazini, imeitaka IAEA kuondosha zile alama na vyombo vya upelelezi vilivyowekwa kwenye kiwanda cha nishati ya nyuklia katika mji wa Yongbyon, mtambo ambao ulifungwa mwaka jana.