Baraza la Usalama linasailia operesheni za UNAMID Darfur
Ijumatatu wajumbe wa Baraza la Usalama walionyesha kuwepo mfarakano na mgawanyika kuhusu suala la kuongeza muda wa vikosi vya mchanganyiko vya Umoja wa Mataifa/Umoja wa Afrika kwa Darfur, yaani vikosi vya UNAMID. Mataifa ya Afrika Kusini na Libya yalipendekeza kuwepo kibwagizo maalumu kwenye azimio la kuongeza muda wa operesheni za vikosi vya UNAMID, kifungu kinachoitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ya Halaiki (ICC) kuakhirisha mashitaka dhidi ya Raisi Omar Al Bashir wa Sudan.