Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa WTO ana matumaini majadiliano yanaingia sura ya kuvutia

Mkuu wa WTO ana matumaini majadiliano yanaingia sura ya kuvutia

Pascal Lamy, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Biashara Duniani (WTO) Ijumatatu aliwaambia waliohudhuria kikao kisio rasmi, Geneva, cha Kamati ya Mapatano ya Biashara ya kwamba ana matumaini kuhusu mwelekeo wa kimawazo kati ya nchi wanachama juu ya suluhu ya zile mada zilizozusha mvutano kwenye majadiliano. Alisema wajumbe waliohudhuria vikao kadha vya mkutano wameonyesha moyo wa kutaka kupatikane suluhu ya kuridhsiha, kwa wote, na hiyo ni ishara nzuri ya kukwamua vizingiti vya hapa na pale vinavyozorotisha majadiloiano, baadhi ya wakati, hususan katika masuala yanayohusu biashara ya kilimo, mathalan, idadi ya kikomo cha ndizi kuuzwa na yale mataifa yenye kuzalisha mavuno hayo.