Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jamii ya kimataifa inahimizwa na KM kuimarisha ari ya Olimpiki

Jamii ya kimataifa inahimizwa na KM kuimarisha ari ya Olimpiki

KM wa UM Ban Ki-moon amewasilisha risala maalumu, kwa kupitia njia ya vidio kuhusu Michezo ya Olimpiki ya mwaka huu itakayofanyika Beijing, Uchina. Risala imependekeza vita isitishwe kote duniani katika kipindi chote michezo ya Olimpiki inafanyika Uchina, kuanzia mwezi Agosti. Kwa mujibu wa risala ya KM, malengo ya maadili ya kimsingi ya Michezo ya Olimpiki hufanana sawa na yale ya UM: hasa katika kukuza mafahamiano na kuhishimiana kati ya wanadamu; na katika majukumu ya kuandalia umma wa kimataifa fursa ya kufanikiwa, kwa usawa, kimaendeleo kwa kufuata taratibu na sheria; na muhimu ya yote katika kuimarisha utulivu na amani kwa wote.