Bei kubwa za chakula zaumiza malhakiri wa ulimwengu, yaonya FAO
Ripoti iliotolewa mjini Roma na Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) iliozingatia matarajio ya akiba ya chakula duniani, imedhihirisha ya kuwa bei kubwa sana za chakula zilizokithiri katika soko la kimataifa sasa hivi, hudhuru zaidi walimwengu wanaoishi kwenye hali duni, umma ambao, ripoti ilitilia mkazo, hulazimika kutumia fungu kubwa la mapato yao kununua chakula.