Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM imewapatia waathiriwa wa zilzala Uchina fedha na mahema 11,000

UM imewapatia waathiriwa wa zilzala Uchina fedha na mahema 11,000

UM umeifadhilia Serikali ya Uchina msaada wa dola milioni 8 kutoka ule Mfuko wa Misaada ya Maafa ya Dharura au Mfuko wa CERF. Msaada huu utakuwa miongoni mwa michango ya kimataifa iliotolewa kuwahudumia kihali waathiriwa wa zilzala iliopiga nchini huko wiki iliopita katika jimbo la kusini la Sichuan, Uchina.