Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mlinda amani wa UNMISS akishika doria katika barabra karibu na Bentiu, jimbo la Unity, Sudan Kusini.
UNMISS Photo

Vikosi vya Umoja wa Mataifa Sudan Kusini vinawapeleka wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.

Walinda amani Sudan Kusini wasindikiza wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.Polisi waliopo kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini  wamepewa jukumu la kuwasindikiza wanafunzi hadi kwenye kituo cha mtihani kwenye mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.  Usindikizaji huo unafanyika Kwa wiki mbili ambapo askari hao wataendelea kuwapeleka na kuwarudisha wanafunzi kufanya mitihani yao kwa usalama.

Sauti
1'57"
Laurent Gbagbo na Charles Blé Goudé wakiwa mahakamani huko The Hague Uholanzi leo tarehe 15 Januari 2019 wakati hukumu ikisomwa. Wameachiwa huru.
ICC-CPI

ICC yawaachia huru Gbagbo na Blé Goudé

Mahakama ya kimataifa ya makossa ya jinai, ICC leo imemwachia huru rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Laurent Gbagbo na aliyekuwa mkuu wa vijana Charles Blé Goudé baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka mashtaka yote dhidi yao. Arnold Kayanda na taarifa zaidi.

Sauti
1'49"
Watoto  wakicheza  kwenye kwenye bomba la maji, kwenye eneo la shule iliyopo katika kambi ya ya wakimbizi wa ndani Bukasi huko Maiduguri nchini Nigeria.
UNICEF/UN055929/Gilbertson VI

Dola milioni 848 zahitajika kunusuru wakimbizi wa ndani kaskazini-mashariki mwa Nigeria

Nchini Nigeria, Kuongezeka kwa mapigano kati ya vikosi vya serikali na makundi yaliyojihami kaskazini mashariki mwezi uliopita wa Desemba na kumesababisha watu wengi zaidi kufurushwa makwao kutoka eneo la Baga na kuelekea kwenye kambi za wakimbizi wa ndani hujo Maiduguri na Manguno ambako tayari  kuna msongamano. John Kibego na taarifa zaidi.

Sauti
55"
Kutoka kushoto: Bendera ya UN ikipepea New York; Naibu Katibu Mkuu akiwa na nakala ya ripoti ya  UNCTAD; Walinda amani wa UN; Katibu Mkuu akiwa na wanawake viongozi waandamizi wa UN
UN

Zilizovuma mwaka 2018

Mwaka 2018 ulighubikwa na changamoto nyingi hususan kwa nchi za Afrika, mizozo ikiendelea kukumba bara hilo sambamba na magonjwa. Hata hivyo kulikuwa na habari chanya, na kwa muhtasari tutaangazia pande zote za sarafu wakati huu ambapo tunafunga mwaka huu wa 2018.

 

Wakimbizi kutoka Iran, Venezuela, Syria, Afghanistan na Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR
UNHCR/UNICEF

Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi kupitishwa leo

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.

 

Mtafiti Rebecca Adami akiwa katika studio za UN News kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.
UN News/Paulina Greer

Wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuandikwa kwa tamko la haki za binadamu

Wiki ijayo, dunia itaadhimisha miaka 70 ya tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu. Ingawa historia ya dunia inaonekana kuwasahau wanawake, mtafiti wa masuala ya haki za binadamu Dkt Rebecca Adami katika kitabu chake cha ‘Wanawake na tamko la haki za binadamu’ anasema wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuliandaa na kulitekeleza tamko hilo.