Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika siku ya kimataifa ya Uhamiaji.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Matafa António Guterres
UNFCCC Secretariat/James Dowson
Katibu Mkuu wa Umoja wa Matafa António Guterres

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika siku ya kimataifa ya Uhamiaji.

Wahamiaji na Wakimbizi

Uhamiaji ni kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi, nguvu na ufahamu. Uhamaji unawaruhusu watu kutafuta fursa mpya, kunufaisha jamii wanakotoka na wanakohamia pia.

Lakini uhamiaji unaporatibiwa vibaya, unaweza kuchochea mgawanyiko katika jamii, kuwaweka watu katika unyonyaji na unyanyasaji na kupunguza imani kwa serikali.

Mwezi huu, dunia ilipiga hatua kwa kuidhinisha mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, uliopangwa vizuri na wa kawaida. 

Mkataba huu ukiwa unaungwa mkono na wanachama wa Umoja wa Mataifa, utatatusaidia kushughulikia changamoto halisi za uhamiaji wakati tukinufaika na faida zake nyingi.

Mkataba huo unatokana na watu na umejikita katika haki za binadamu.

Unaonesha njia za kuelekea kwenye fursa halali kwa uhamiaji na hatua madhubuti za kupambana na usafirishaji haramu wa wanadamu.

Katika siku ya kimataifa ya uhamiaji, tufuate njia iliyowekwa na azimio hili la ulimwengu ili uhamiaji unufaishe watu wote.

Tafadhali iwapo unataka kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa, tafadhali jisajili na pia unaweza kupakua apu ili kuweza kusikiliza wakati wowote popote ulipo.