Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Udongo wenye rutuba husaidia kilimo bora cha migomba kama vile mkoani Kagera nchini Tanzania
UNDP SGP Panama/Andrea Egan

Ulemavu sio kulemaa, ninachohitaji ni kuwezeshwa:Mkulima Gideon Masinde

Ingawa hali ya ulevu hasa wa viungo mara nyingi huleta changamoto kwa muhiska kuanzia  katika maisha ya kawaida na hata katika kujikwamua kiuchumi jambo ambao huwafanya wengi wasio na msaada kuishia kuwa ombaomba, au kukabiliwa na hali ngumu sana. Lakini kama walivyonena wahenga penye njia pana njia , kauli inayothibitishwa na Gideon Malungula Masinde mwenye umri wa miaka 42 ambaye ana ulemavu wa miguu yote na hawezi kusimama wa wala kutembea lakini hakuacha ulemavu wake umlemaze zaidi. 

Sauti
2'55"
Waziri wa afya maendeleo ya jamii wazee na watoto wa nchi hiyo Ummy Mwalimu akizungumza na Flora Nducha wa UN News kandoni mwa mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani kikao cha 63
UN News Kiswahili/ Grece Kaneiya

Bila ushiriki wa wanawake hatutakuwa na Tanzania ya viwanda:waziri Mwalimu

Serikali ya Tanzania imesema bila ushiriki kamilifu wa wanawake haitoweza kutimiza azma ya kuwa na maendeleo ya viwanda itakayoleta tija kwa wote.

Kauli hiyo imetolewa na waziri wa afya maendeleo ya jamii wazee na watoto wa nchi hiyo Ummy Mwalimu akizungumza na Flora Nducha wa UN News kandoni mwa mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani kikao cha 63 kinachoendelea kwenye mako makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani na kuongeza kuwa na huo ndio ujumbe wao pia kwenye mkutano huu

(MAHOJIANO NA UMMIE MWALIM)

Sauti
2'10"
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa amataifa la wanawake-UN-Women,Phumzile Mlambo-Ngcuka,(kushoto) akiwa na wanawake wmjini Baidoa Somalia.
UN Women/Patterson Siema

Hatuwezi kutothamini mchango wa nusu ya watu duniani :Guterres

Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambayo kila mwaka huwa Mach inane wito umetolewa kuhakikisha uwezeshaji wanawake na usawa jinsia vitu ambavyo ni muhimu kwa maendeleo ya dunia. Wito huo umetolewa na viongozi mbalimbali wanawake kwenye Umoja wa Mataifa lakini pia Katibu Mkuu Antonio Guterres. Kaulimbiu ya mwaka huu ikiwa ni “fikra sawa, jenga kwa ufanisi na kuwa mbunifu kwa mabadiliko 

Sauti
3'
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika mgogoro wa jina katika ya Ugiriki na Macedonia iliyokuwa Jamhuri ya Yugoslavia (FYROM), Matthew Nimetz
UN News/Video capture

Kukata tamaa sio hulka yangu: Nimetz

Mwezi Juni mwaka jana mkataba wa kihistoria ulimaliza mgogoro wenye utata wa miaka 27 kati ya nchi mbili, ambazo ni jamhuri ya Yugoslavia ya zamani na Ugiriki. Mwanaume mmoja Matthew Nimetz kwa uvumilivu na hekma aliongoza majadiliano kwa niaba ya Umoja wa Mataifa kwa zaidi ya miongo miwili na akizungumza na UN News amesema Imani yake ya matokeo chanya katika mchakato huo haikuwahi kutoweka.

Sauti
4'16"