Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Kamanda wa kikosi cha TANZBATT 9 akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Jengo la eneo la chakula lililokabidhiwa na walinda amani wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kwa Zahanati ya Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu kaskazini mashariki mwa jamhuri ya…
TANZBATT 9 / Private Sosper Msafiri

Kampeni ya Amani na Afya ya TANZBATT 9 nchini DRC yahitimishwa kwa kukabidhi jengo

Kikosi cha 9 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupitia Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo - MONUSCO wamehitimisha kampeni yao ya Afya na Amani iliyoanza tarehe 3 mwezi huu wa January ambapo  wamekabidhi jengo kwa ajili ya mahali pa wagonjwa na wahudumu wa afya kula chakula katika Kituo cha Afya cha Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.

Sauti
3'55"
Kundi la wakimbiziwakishuka kutoka kwa boti lililokuwa limejaa maji baada ya kufika katika kisiwa cha Ugiriki cha Lesvos (30 Septemba 2015).
Photo: UNHCR/Achilleas Zavallis

Mashtaka yote dhidi ya wanaookoa wahamiaji baharini huko Ugiriki yafutwe- OHCHR

Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kesi iliyoanza huko Lesvos nchini Ugiriki dhidi ya watetezi 24 wa haki za binadamu wanaoshtakiwa kwa kutekeleza jukumu la kuokoa wahamiaji ambao walikumbwa na zahma baharini wakati wakikimbilia barani Ulaya kusaka maisha bora. Kesi hiyo imeanza wiki hii baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu.

Sauti
2'12"
Uchunguzi wa virusi vya Ebola kwenye mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo , DRC na Uganda
WHO/Matt Taylor

Uganda yatangaza kutokomezwa kwa mlipuko wa Ebola

Uganda hii leo imetangaza kutokomeza mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliosababishwa na virusi aina ya Sudan, ikiwa ni chini ya miezi minne tangu kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza kwenye wilaya ya Mubende nchini humo 20 mwezi Septemba mwaka jana. Taarifa ya Thelma Mwadzaya inafafanua zaidi. 

 

Sauti
2'27"
Walinda amani kutoka Tanzania waanzisha kampeni ya "Afya na Amani" nchini CRC
Picha: MONUSCO

Baada ya Mavivi, walinda amani wa UN kutoka Tanzania wafikisha misaada Hospitali ya Oicha, DRC

Kikosi cha 9, TANZBATT 9 cha wanajeshi walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo DRC-MONUSCO, wameendelea na kampeni yao ya Afya na Amani ambapo hadi tarehe 13 mwezi huu wa Januari watakuwa wakiendelea kutoa misaada kwa jamii inayoishi katika eneo lao la kazi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Sauti
2'13"