Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Wanawake katika kambi ya Dadaab nchini Kenya
UN Women

Wanawake Dadaab Kenya wajumuika kukabili misimamo mikali

Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women kwa ushirikiano na wadau wanajengea uwezo wajenzi wa amani mashinani hata kwenye maeneo yenye changamoto kama vile kambi ya wakimbizi ya Daadab kwenye kaunti ya Garissa nchini humo kwa lengo la kuepusha vijana kutumbukizwa kwenye vikundi vyenye msimamo mkali.

Sauti
2'15"
Ina Maria Shikongo, mwanaharakati wa watu wa jamii ya asili kutoka Namibia akiwa kwenye maandamano huko COP27 Sharm-el-Sheikh nchini Misri.
UN News/Laura Quinones

Wanaharakati huko COP27 wasema hakuna hatua kwa tabianchi bila kujali haki za binadamu

Huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri, kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, tarehe 17 mwezi huu wa Novemba yalishuhudiwa maandamano ya maelfu ya wawakilishi wa watu wa jamii ya asili, wanawake, wanarahakati wa masuala ya jinsia, vijana, mazingira na haki kwa tabianchi kutoka pande mbalimbali za dunia.

Sauti
3'51"
Michael Dunford, Mkurugenzi wa WFP Pembe ya Afrika akihojiwa na UN News.
UN/ Leah Mushi

Hatari ya baa la njaa bado ni jinamizi linaloizonga Somalia: WFP Dunford

Ukame uliolighubika eneo la Pembe ya Afrika kwa miongo minne mfululizo umesababisha changamoto kubwa kwa mamilioni ya raia wa Kenya, Ethiopia na Somalia nchi ambayo maeneo mengi yanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula na hatihati ya kutumbukia kwenye baa la njaa. Mashirika ya misaada ya kibinadamu likiwepo la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP yako mstari wa mbele kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani wa chakula.

Sauti
2'
Sedelia Abdullahi ni mhudumu wa afya wa mstari wa mbele huko mashinani nchini Ethiopia na kila siku huchunguza na kutibu watoto wenye utapiamlo kwenye kituo cha afya cha kambi ya wakimbizi ya Bambassi nchini Ethiopia kilichojengwa na UNICEF kwa ufadhili …
UNICEF Ethiopia

Wahudumu wa afya Ethiopia warejesha tabasamu kwa watoto- UNICEF

Nchini Ethiopia, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniain, UNICEF kupitia msaada kutoka Muungano wa Ulaya umewezesha mamia ya wahudumu wa afya walio mstari wa mbele kila uchao kuweza kutembelea wakimbizi wa ndani waliofurushwa makwao kutokana na mzozo kwenye jimbo la Benishangul-Gumuz lililoko kaskazini-magharibi mwa taifa hilo, likipakana na Sudan ili kuwapatia huduma za lishe bora wakati huu ambapo watoto wanakabiliwa na utapiamlo.

Sauti
2'31"
Emmanuel Cosmas Msoka, Mchechemuzi wa Vijana wa UNICEF Tanzania kuhusu usafi wa maji, usafi wa mazingira (WASH) na ubunifu.
UN/Anold Kayanda

Maneno ni bei nafuu sana lakini vitendo ni bei ghali, tushirikishe vijana kwa vitendo:Msoka  

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu leo unakunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York Marekani. Mkutano huo wa siku tatu umeitishwa ili kukabiliana na changamoto ya kimataifa ya elimu hasa kwa kuzingatia suala la usawa na ujumuishwaji, ubora wa elimu na umuhimu.  

Sauti
2'23"
Taswira wa darasa la mfano linalolenga kuonesha Mgogoro wa kujifunza duniani. Darasa hili lililoandaliwa na UNICEF liko makao makuu ya UN jijini New York, Marekani.
© UNICEF/Chris Farber

Mtoto 1 kati ya 3 duniani kote ndiye awezaye kusoma na kuelewa hadithi fupi na hali si shwari - UNICEF

Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani ukianza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limetoa taarifa inayoeleza idadi ya Watoto wasiojua kusoma imeongezeka ulimwenguni ikilinganishwa na miaka miwili iliyopita. 

Sauti
2'31"
Waathirika wa mafuriko kwenye eneo la Balochistan, nchini Pakistani.
WFP Pakistan

Msifurishe dunia hii leo, wala msiizamishe kesho- Ujumbe wa Katibu Mkuu wa viongozi wa dunia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani hii leo ikiwa ni kuelekea Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la UN unaoanza wiki ijayo akisema ujumbe wake mkuu kwa viongozi watakaoshiriki ni dhahiri ya kwamba wachukue hatua kupunguza kiwango cha joto duniani.

Sauti
3'45"