Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Katibu Mkuu  António Guterres ametembelea maonesho ya picha ya "Mikononi mwao: Wanawake wachukua umiliko wa amani" katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa
UN Photo/Mark Garten)

Muda wa kurudisha nyuma saa ya haki za wanawake umepita, sasa iende mbele- Guterres alieleza Baraza

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu wanawake, amani na usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati umefika kwa baraza hilo kuonesha kwa vitendo uungaji wake mkono wa harakati za wanawake katika ujenzi na uendelezaji wa amani badala ya kusalia maneno matupu.  Flora Nducha na maelezo zaidi.

Sauti
3'18"
Maza, ng'ombe ambaye amebadili maisha ya familia maskini nchini Burundi
@UNICEFBurundi/2021/Hamburger

Ng’ombe mmoja aleta hakikisho la maisha kwa kaya maskini Burundi

Mtamba mmoja wa ng’ombe anaweza kuonekana si chochote kitu kwa wafugaji wabobezi lakini kwa Beatrice Nibogora na familia yake nchini Burundi, mtamba huyo akipatiwa jina Maza amegeuka lulu na ufunguo wa maisha yenye matumaini na kutimiza methali ya wahenga ya kwamba baada ya dhiki ni faraja. Hii ni baada ya mradi wa Benki ya Dunia na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kubisha hodi kunusuru kaya maskini.

Sauti
1'58"
Mlima Kilimanjaro ulioko Tanzania
World Bank/Curt Carnemark

Watu mashuhuri 34 wanapanda mlima Kilimanjaro ili kuchagiza usawa wa chanjo ya COVID-19:

Wapanda mlima 34 leo wameanza safari ya kupanda mlima mrefu zaidi barani Afrika , mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuchagiza upatikanaji wa chanjo ya COVID-19 kwa wote. Kundi hilo linalojumuisha watu kutoka katika nyanja za biashara, serikali, wanamichezo mashuhuri na wawakilishi wa vijana linatarajiwa kuwasili kwenye kilele cha mlima huo tarehe 24 Oktoba siku ya Umoja wa Mataifa.

Sauti
3'8"