Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mamilioni ya watu nchini Bangladesh wameathirika na mabadiko ya tabianchi, mafuriko ikiwa moja ya atahri hizo
WFP/Sayed Asif Mahmud

Wakulima wanabeba gharama kubwa ya mabadiliko ya tabianchi Bangladesh:IFAD

Nchini Bangladesh mabadiliko ya tabianchi yamekuwa ni mwiba kwa maisha ya kila siku ya watu wa taifa hilo la Asia. Kwa mujibu wa mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD zaidi ya nusu ya watu milioni 90 wa nchi hiyo wanaishi katika maeneo yaliyoathirika vibaya na mabadiliko ya tabianchi huku wakikabiliwa na hatari kubwa ya mafuriko na wakulima ndio wanaobeba gharama kubwa ya zahma hiyo. 

Sauti
2'36"
Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya changamoto zinazoikabili dunia. Ukanda wa Saheli kusini mwa jangwa la Sahara.
© UNDP Mauritania/Freya Morales

Kama sisi tumeweza, wengine washindwe kwa nini? – Wakimbizi Mauritania 

Hivi karibuni, siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mabadiliko ya tabianchi, #COP26 ambao hivi sasa unaendelea Glascow, Uskochi, Mshauri Maalumu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudunia wakimbizi, UNHCR kuhusu Hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi, Andrew Harper ametembelea Mauritania kujionea jinsi wakimbizi wanavyopambana na janga la tabianchi.

Sauti
2'5"
Mwandishi wa habari akichukua tukio kwa video
Unsplash/Jovaughn Stephens

Ulinzi kwa waandishi wa habari unahitaji utashi wa kisiasa: UN

Pamoja na kufanya kazi kubwa ya kuhabarisha umma, waandishi wa habari ulimwenguni kote wanakabiliwa na mashambulio yanayohatarisha usalama wao ambapo mashambulio hayo ni pamoja na kauli za chuki, udhalilishaji kwenye mitandao ya kijamii, vurugu, ubakaji na hata mauaji.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukomesha uhalifu dhidi ya waandishi wa habari Umoja wa Mataifa unasema muarobaini wa yote hayo ni utashi wa kisiasa.

Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa (ILO) linakadiria kuwa watoto milioni 168 duniani kote - mmoja kati ya kumi - wanashiriki katika ajira za utotoni
UN Photo/Martine Perret

Mtoto 1 kati ya 10 duniani watumikishwa katika ajira ya watoto:FAO/ILO

Leo hii kote duniani mtoto 1 kati ya 10 anatumikishwa katika ajira ya watoto na asilimia kubwa katika sekta ya kilimo ambao ni jumla ya watoto milioni 112 sawa na asilimia 70 ya watoto wote walio katika ajira, limesema leo kongamano la kimataifa lililoandaliwa kwa njia ya mtandao na shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO kwa lengo la kusaka suluhu za kutokomeza ajira hiyo.

Viwanda vikubwa hutoa hewa chafuzi ambayo inasababisha shida kadhaa za kiafya.
Unsplash/ Sergio Rodriguez

Nchi nyingi hazijawasilisha rasmi ahadi mpya za kupunguza hewa chafuzi:UNEP

Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP imeeleza kuwa ahadi mpya na zilizorekebishwa kuhusu viwango vya nchi vya kukabili mabadiliko ya tabianchi, NDCs hazijafikia lengo lililowekwa katika mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi na hivyo ulimwenguni kuwa hatarini kuwa na ongezeko la joto la angalau nyuzijoto angalau 2.7 katika karne hii.

Sauti
1'17"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kushoto) na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya mazungumzo jijini New York, Marekani.mwezi Septemba 2021 (Maktaba)
UN / Evan Schneider

Tumeomba mazungumzo na UN wasaidie hali Burundi ili kuandaa Tanzania  kuwarejesha wakimbizi - Rais Samia 

Tanzania ni moja ya nchi za Afrika mashariki ambazo zimekuwa kimbilio la wakimbizi kwa miaka mingi. Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan alipozungumza na Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alipokuwa hapa New York, Marekani anasema ni takribani miaka 50 kwa nyakati tofauti nchi yake imekuwa ikipokea wakimbizi na kwa sasa ameomba mazungumzo na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la kuhudumia wakimbizi UNHCR kusaidia katika nchi wanakotoka wakimbizi ili waweze kurejea akitolea mfano Burundi.

Sauti
2'57"