Jina la ndui ya nyani au Monkeypox linabadilishwa kuepusha unyanyapaa- WHO
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, liko kwenye mchakato wa kubadilisha jina la ugonjwa wa ndui ya nyani au Monkeypox.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, liko kwenye mchakato wa kubadilisha jina la ugonjwa wa ndui ya nyani au Monkeypox.
Katika kuchukua hatua za dharura kusaidia jamii zilizoathiriwa na mafuriko nchini Yemen, shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limepeleka msaada wa dharura wa vifaa vya matibabu ikiwemo maabara kwa lengo la kuinua uwezo wa timu zinazotoa huduma za waathirika wa mafuriko waliopata kiwewe
Pembe ya Afrika hali ya ukame inazidi kutishia uwezekano wa baa la njaa kwenye eneo hilo linalojumusha Kenya, Somalia na Ethiopia huku Umoja wa Mataifa ukisema takribani watu milioni 18.4 huamka kila siku bila uhakika wa mlo huku idadi hiyo ikitarajiwa kufikia milioni 20 mwezi ujao wa Septemba. Wanawake na watoto wameathirika zaidi ambapo kando ya njaa wanakumbuka kile walichokuwa wanafanya hali ilivyokuwa nzuri na wanatamani hali hiyo irejee.
Kampuni ya kutengenza dawa za binadamu ya GSK imepatiwa kandarasi ya kuzalisha chanjo ya kwanza ya Malaria duniani lengo likiwa ni kulinda mamilioni ya watoto dhidi ya ugonjwa huo unaogharimu mamilioni ya Maisha ya watoto limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF hii leo.
Meli ya kwanza ya Ukraine yenye na unga wa ngano wa Ukraine utakaosambazwa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP kwenye operesheni zake za kibinadamu imeondoka bandari ya Yuzhny nchini Ukraine hii leo, hatua ambayo imetajwa kuwa ya muhimu zaidi na inayohitajika ya kuondoa nafaka kwenye taifa hilo lenye mzozo kuelekea nchi zinazokumbwa na janga la uhaba wa chakula duniani.
Katikati ya mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kuna vioski lukuki vya kutengeneza simu janja na miongoni mwao ni cha vijana wawili wanufaika wa mradi wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, mradi wa kupunguza ghasia, CVR katika taifa hilo lililoghubikwa na ghasia mashariki mwa nchi.
Kutoka Ethiopia hadi Chad na Palestina, Elimu haiwezi kusubiri au ECW , ni mradi wa Umoja wa Mataifa wa elimu katika maeneo yenye dharura na migogoro ya muda mrefu, ambao umesaidia mamilioni ya wavulana na wasichana walioathiriwa na migogoro duniani kote kutimiza ndoto zao.
Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS wanafanya kazi ya kuondoa maji ya mafuriko yaliyotwama katika eneo kubwa la mji wa Bentiu jimbo la UNITY ili kuhakikisha uwanja wa ndege na barabara zinazopatakana na uwanja huo zinapitika.
Mwaka mmoja tangu watalibani watwae madaraka nchini Afghanistan, shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake duniani, UN-Women hii leo limesihi mamlaka hizo kufungua shule kwa ajili ya watoto wote wa kike, ziondoe vikwazo vya ajira kwa wanawake na ushiriki wao kwenye siasa za taifa hilo sambamba na kufuta sera zote zinazowanyima wanawake na wasichana haki zao.
Mwaka mmoja tangu watalibani wachukue madaraka nchini Afghanistan, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF, limesema kitendo cha Watoto wa kike kuenguliwa kwenye masomo kimegharimu asilimia 2.5 la pato la ndani la taifa hilo la barani Asia.