WHO yaonya juu ya hatari ya mlipuko wa magonjwa huku mafuriko yakiendelea Pakistan
Hatari kubwa za kiafya zinajitokeza nchini Pakistan huku mafuriko ambayo hayajawahi kushuhudiwa yakiendelea, limeonya leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa ulimwenguni (WHO)na kuongeza kuwa kuna hatari ya kuzuka na kuenea kwa magonjwa ya malaria, homa ya kidingapopo na magonjwa mengine yanayoenezwa na maji na wadudu.