Tuko tayari kusaidia waathirika wa machafuko Ukraine:Mashirika ya UN
Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la mpango wa chakula duniani WFP, la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la elimu sayansi na utamaduni UNESCO, pamoja na kutiwa hofu kubwa na kulaani kinachoendelea nchini Ukraine, yamesema yako tayari kusaidia kwa hali na mali waathirika wa machafuko hayo nchini Ukraine