Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hawa Hussein Njolo, aliyekuwa anatekeleza FGM, ambaye pia yeye mwenyewe ni muathirika wa ukeketaji.
Screenshot

Nilikeketwa, nikakeketa, nimeyaona madhara nimeacha – Aliyekuwa ngariba

Ingawa mila hii ya ukeketaji imekuwepo kwa zaidi ya miaka elfu moja, Umoja wa Mataifa unaamini kwamba mila hii iliyopitwa na wakati inaweza kutokomezwa katika kizazi kimoja. Ndio maana Umoja wa Mataifa unajitahidi kutokomeza kikamilifu matendo hayo katika muongo huu kufikia mwaka 2030, kwa kufuata mwelekeo wa Lengo la 5 la Maendeleo Endelevu linalolenga usawa wa kijinsia.