Kituo cha kutibu Ebola Butembo chashambuliwa, UNICEF yafunguka
“Nachukizwa na shambulio la hivi karibuni zaidi dhidi ya kituo cha kutibu Ebola huko Butembo, jimbo la Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC,” ndivyo ilivyoanza taarifa iliyotolewa jioni ya leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, mjini New York, Marekani.