Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa katika mahojiano maalumu na Mkuu wa Idara ya mawasiliano ya umma ya Umoja wa Mataifa Melissa Fleming mjini New York Marekani Septemba 18, 2019.
UN News/Ben Lybrand

Kutowashirikisha vijana kwenye tabianchi ni janga- Guterres

Kuelekea siku ya kimataifa ya amani ambayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 21, leo katika maadhimisho kwenye Umoja wa Mataifa Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa kukabiliana na changamoto kubwa za dunia ikiwemo mabadiliko ya tabianchi ili kudumisha amani kwa wote. 

Sauti
3'12"
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, David Shearer akihutubia Baraza la Usalama.
UN Photo/Ariana Lindquist

Mchakato wa amani Sudan Kusini unahitaji u tayari wa pande husika na msaada wa jamii ya kimataifa-Shearer

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, David Shearer amesema mchakato wa amani nchini humo unasalia kuwa, “hatarini, lakini hatua zinapigwa, ” akiongeza kuwa hatua zinategemea u tayari wa pande husika na uungwaji mkono na jamii ya kimataifa katika kuunda serikali ya mpito.

Makubaliano ya kihistoria ya kuhuisha amani Sudani Kusini yatiwa saini kati ya rais Salva Kiir (kulia) na kiongozi wa upinzani Riek Machar, pichani ewakishikana mikono mjini Addis Ababa 12/9/2018
UNMISS\Nektarios Markogiannis

Awamu ya pili ya majadiliano ya kuunda serikali mpya Sudan Kusini yamefanyika mjini Juba

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na aliyekuwa naibu wake Riek Machar wamekamilisha majadiliano ya siku ya pili mjini Juba nchini Sudan Kusini huku viongozi hao wawili wakirejelea azma ya kufikia amani huku wakiahidi kukutana mara kwa mara kuelekea uundaji wa serikali ya mpya ya umoja wa kitaifa inayotarajiwa Novemba 12 mwaka huu 2019.

Sauti
2'43"