Mkutano wa Kiir na Machar umerejesha imani Sudan Kusini- Deng Gai
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo limejulishwa kuwa mkutano kati ya Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini na mpizani wake Riek Machar kwenye mji mkuu Juba hivi karibuni ulikuwa ni fursa pekee ya kutatua masuala muhimu ambayo hayajapatiwa ufumbuzi kwenye mzozo unaoendelea nchini humo.