Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sudan Kusini

Baada ya kuporwa utoto wao na vita, sasa maelfu ya watoto waishia ukimbizini Uganda

Wahudumu wa mashirika ya misaada ya kibinadamu nchini Uganda wakiwemo wa Umoja wa Mataifa wanakumbana na changamoto kubwa ya kuwasaidia watoto wakimbizi zaidi ya 25,000 waliotengana na wazazi ama walezi wao kutokana na vita na kusaka hifadhi wakiwa peke yao nchini humo. Mwandishi wetu wa Uganda  John Kibego ametembelea makazi ya wakimbizi ya Imvepi Wialayani Arua nchini humo ambako kuna asilimia kubwa ya watoto  na kuandaa tarifa hii.

Mkimbizi wa ndani Sudan Kusini akiwa na virago vyake kufuatia ghasia zinazoendelea nchini humo. UNMISS (Maktaba)
UNMISS (Maktaba)

Nilichoshuhudia kinakatisha tamaa- Shearer

Kufuatia mapigano ya hivi karibuni huko Sudan Kusini yaliyosababisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo David Shearer amezuru maeneo hayo na kushuhudia hali halisi ikiwemo mtoto aliyenusurika kifo baada ya kupigwa risasi.

Sauti
1'39"