Kasi ya ukatili wa kingono Somalia inatisha- UN
Ongezeko la kutisha la asilimia 80 la vitendo vya ukatili wa kingono nchini Somalia limewekwa bayana katika ripoti mbili za hivi karibuni za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambapo hii leo wawakilishi wake maalum wamesema ni jambo la kusikitisha.