Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Mwanamke na watoto wake wakiwa wamesismama kwenye mlango wa makazi yao ya muda kwenye mji wa Ibb Yemen :Kutoka maktaba
IOM/Olivia Headon
Mwanamke na watoto wake wakiwa wamesismama kwenye mlango wa makazi yao ya muda kwenye mji wa Ibb Yemen :Kutoka maktaba

Takriban Wakimbizi 300,000 wapata maambukizi ya virusi vya Corona mwaka 2020

25 Mei 2021
Wahamiaji na Wakimbizi

Takriban wakimbizi 300,000 kutoka Mashariki na Pembe ya Afrika, wamepata maambukizi ya virusi vya Corona au COVID-19 kwa mwaka 2020. Idadi hiyo imetajwa kwenye ripoti kuu ya mwaka 2020 ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM, kwa bara la Afrika iliyotolewa wiki hii.

Taarifa ya IOM kutoka Nairobi Kenya, imeangazia matokeo mabaya ya janga la Corona kwa wahamiaji walio kwenye mazingira magumu, wahamiaji wa ndani, wakimbizi wanaotafuta hifadhi, watoto walio peke yao, wakimbizi wanaorudi na wale waliokwama.

Mohammed Abdiker, Mkurugenzi wa IOM, Kanda ya Mashariki na Pembe ya Afrika amesema, "Tunaposonga mbele tunatakiwa kuimarisha njia za uhamiaji wa kawaida na kuhamasisha uendelezaji wa wahamiaji wanaorejea nyumbani".

Maelfu ya wakimbizi, wengi wao kutokea Ethiopia wamekwama huko Djibouti, Somalia na Yemen, wakishindwa kuendelea na safari yao ya kwenda Saudi Arabia kupitia Yemen. Kwa mujibu wa taarifa, idadi ya watu wanaovuka Yemen kutokea Pembe ya Afrika imepungua kwa kiwango kikubwa, kutoka watu 138,000 hadi watu 37,000 sawa na upungufu wa zaidi ya asilimia 73 ikilinganishwa na mwaka 2019.

Abdiker amesema ili suluhu ipatikane ni lazima udhibiti wa wahamiaji kuimarishwa, "Tunahitaji kuona juhudi za kudhibiti uhalifu wa kikanda na kimataifa ambao utahusisha usafirishaji wa wakimbizi na utoroshaji wa watu katika Kanda. Bila ya hivi juhudi zinazofanywa na nchi wanachama kudhibiti uhamiaji zitaendelea kudhoofishwa na wahamiaji wataendelea kuteseka"

Mamia ya maelfu ya watu katika ukanda wa mashariki na Pembe ya Afrika wanaupungufu wa chakula, maji, ulinzi na dawa. Pia vifaa vya kujilinda dhidi ya maambukizi ya COVID19 ni vichache na kwasasa hawana namna ya kufikiwa na chanjo ya Corona.

Ripoti hiyo imehitimisha kwa kusema wakati chanzo cha wakimbizi kwa Upande wa Mashariki na Pembe ya Afrika ni umasikini, machafuko na matukio yanayosababishwa na athari za mazingira, janga la Corona limeongeza tabu Zaidi kutokana na uchumi kuathirika vibaya.

Hoja ya ripoti hiyo ya IOM inaungwa mkono na ripoti ya hivi karibuni ya Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa ambayo limeeleza athari za muda mrefu za kiuchumi na kijamii zilizosababishwa na COVID-19 zitaongeza wigo wa umaskini baina ya nchi na athari Zaidi zinaelezwa zitatokea kwa watu waishio barani Afrika.

 

♦ Kurambaza ukurasa mahsusi wa Siku ya Kiswahili Duniani bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
wakimbizi|wahamiaji|COVID-19|Corona

Taarifa Zihusianazo

Watu walioshikiliwa kwenye mji mkuu wa Libya, Tripoli, wakisubiri kuhamishiwa eneo salama. Pichani Msichana kutoka Eritrea mwenye umri wa miaka 19 akizungumza na mfanyakazi wa UNOCHA akisubiri kupanda basi kuelekea kituo cha mpito kabla ya kwenda Niger.

Mapigano yakiendelea Tripoli, wakimbizi 131 wasafirishwa kwenda Niger

Wakimbizi na watoto wahamiaji waishio katika kituo cha mapokezi Moria, sehemu za Lesvos, Ugiriki

UNHCR yataka Ulaya ichukue hatua kulinda watoto wakimbizi

Kinamama na watoto wakimbizi wa ndani katika kituo kimoja wakiuza bidhaa zao kujipatia pato .

Viongozi wa Afrika wanusuruni watoto milioni 13.5 waliofurushwa makwao– UNICEF

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials