UNICEF Zambia yatumia WASH kunusuru wakimbizi na wenyeji
Nchini Zambia shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limechukua hatua kusaidia jimbo la Luapula lililoko mpakani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kuwa na huduma za kujisafi na maji safi, WASH kwa lengo la kuondokana na magonjwa ya kuambukiza na pia kupatia watoto fursa ya kutosha ya kujifunza.