Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Wanawake wakiwa wamekusanyika katika kituo cha kugawa chakula cha Nyanzale Kivu Kaskazini DRC. Kituo hicho kinawalenga kwa msaada familia zisizojiweza na zilizo hatarini
OCHA/Ivo Brandau

Mashirika ya UN yaendelea kufikisha nuru kwa wakimbizi huko Ituri DRC 

Katika jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Umoja wa Mataifa kupitia mashirika yake umeendelea kusambaza misaada kwa wakimbizi wa ndani ambao walilazimika kukimbia makwao na kuacha kila kitu na hivi sasa wanaishi kwenye kambi za wakimbizi hususan katika eneo la Pinga jimboni humo. Misaada hiyo imekuwa jawabu kwa wakimbizi ugenini.

Sauti
2'35"
Anwarita akiwa nyumbani kwa wazazi wake walezi huko Bona, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
© UNICEF/Roger LeMoyne

"Nilisikia sauti usiniache! ndipo nikakuta mtoto Anuarita"- Asema baba aliyenusuru mtoto msituni huko DRC

Anwarita mtoto mwenye  umri wa miaka 8 amejikuta yatima baada ya waasi kuua kwa mapanga wazazi wake huko Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Hivi sasa Anwarita anaishi na familia iliyomnusuru msituni, wakati huu ambapo takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linasema kwa sasa watoto milioni 3 nchini humo wametawanyishwa na mizozo.