MONUSCO yapatia maafisa na askari wa jeshi la DRC pamoja na polisi mbinu za medani
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepatia mafunzo ya mbinu za medani na usimamizi wa vilipuzi sambamba na ufyatuaji wa risasi, maafisa na wanajeshi 652 wa vikosi vya jeshi la serikali, FARDC na jeshi la polisi kama njia mojawapo ya kuimarisha ulinzi nchini humo.