Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Charlotte Fatuma, mkimbizi kutoka DRC anaendesha duka kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Coranne nchini Msumbiji kutokana na umeme ambao umefanikishwa na mradi unaotekelezwa na UNHCR, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
UNHCR Video

Utu na maendeleo vyakutanishwa Coranne na kuleta ustawi kwa wakimbizi na wenyeji

Charlotte Fatuma na Neema Cenga ni wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na sasa wanaishi ukimbizini nchini Msumbiji katika jimbo la Nampula. Kwa sasa Charlotte ni mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa, akiendesha biashara ya duka kwenye makazi ya wakimbizi ya Coranne huku Neema naye akijitahidi kulea na kusomesha watoto wake.  

Sauti
4'28"
Tukio la kuwaaga walinda amani wa MONUSCO waliokufa wakati wa maandamano na uvamizi wa vituo vya ujumbe huo huko Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini. (1 Julai 2022)
UN/Byobe Malenga

Walinda amani wa MONUSCO waliouawa katika maandamano DRC waagwa 

Viongozi wa Umoja wa mataifa pamoja na serikali ya Jamhuri ya Kidemoktrais ya Congo, DRC wametoa heshima zao za mwisho kwa walinda amani watano wa kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO waliokufa wakati wa maandamano na uvamizi wa vituo vya ujumbe huo huko Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini. Walinda amani hao wanatoka Morocco na India ambapo Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Bintou Keita amesema MONUSCO iko tayari kwa mazungumzo ya amani ili kuendeleza na kudumisha amani nchini humo.

Sauti
2'29"
Naibu Mwakilisih wa Katibu Mkuu wa UN nchini DRC Kassim Diagne akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 26 Julai 2022, mkutano  ulihudhuriwa pia na Msemaji wa Serikali ambaye pia ni Waziri wa Habari Patrick Muyaya.
UN/Boybe Malenga

Vurugu dhidi ya ofisi za UN DRC: Serikali kuwasaka na kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imesihi utulivu miongoni mwa wananchi baada ya maandamano na uvamizi dhidi ya vituo vya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kwenye miji ya Goma na Butembo jimboni Kivu Kaskazini, tukio ambalo hata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka mamlaka zichunguze na sheria ichukue mkondo wake. Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ana taarifa zaidi.

Sauti
3'22"
Mfanyabiashara barabarani akiuza chakula barani Afrika
IMF

Dunia kushuhudia kudorora zaidi kwa uchumi: IMF

Ripoti ya hali ya uchumi kwa robo ya pili ya mwaka huu wa 2022 ambao ni mwezi Aprili hadi Juni ambayo imetolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa IMF imesema matarajio ya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kukumbwa na kiza na yanakosa uhakika na kwamba matumaini ya uchumi kukwamuka mwaka 2021 yanazidi kuyoyoma mwaka huu wa 2022. 

Sauti
2'34"
Kambi ya wakimbizi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNOCHA

Mkutano wa kirafiki wakutanisha walinda amani kutoka Tanzania na baadhi ya viongozi mashariki mwa DRC

Kuelekea siku ya kimataifa ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa na katika kuendeleza jukumu la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  vikosi vya ulinzi wa amani kutoka Tanzania yaani TANZBATT 9 na kikosi cha utayari TANZANIA QRF2 vimefanya kikao cha Urafiki baina yao na uongozi wa raia wa nchi hiyo katika maeneo ya uwajibikaji wa vikosi hivyo.

Sauti
3'17"