Idadi kubwa ya watoto katika maeneo ya Ebola DRC wamerejea shuleni:UNICEF
Mwezi mmoja baada ya kuanza kwa mwaka mpya wa masomo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, asilimia 80 ya watoto wenye umri wa kwenda shule kwenye maeneo ya Beni na Mabalako huko jimbo la Kivu Kaskazini ambayo yalikuwa kitovu cha mlipuko wa sasa wa Ebola, tayari wamerejea shuleni.