Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DR Congo

Askari wa kikosi cha FIB akishika doaria  Beni Mashariki mwa DRC ambapo UN ilikuwa inasaidia jeshi la serikali katika operesheni zake.
Photo: MONUSCO/Sylvain Liechti

Mashambulizi dhidi ya raia yaongezeka Beni: UNHCR

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limesema lina wasiwasi kuhusu usalama wa maelfu ya raia katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, DRC ambako ghasia za makundi yenye silaha zimeongezeka na za hivi karibuni zimesababisha vifo vya watu zaidi ya 20. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.

Afisa wa UNICEF azungumza na watoto kuhusu umuhimu wa kuzuia Ebola karibu na Mangina, Kivu Kaskakzini ,DRC
UNICEF/Mark Naftalin

Ebola sasa iko Butembo,  mashariki mwa DRC- UNICEF

Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa la UNICEF linapanua wigo wa operesheni zake za kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,  DRC baada ya serikali kuthibitisha kuwepo kwa wagonjwa wapya wawili  kwenye mji wa Butembo, jimboni Kivu Kaskazini.