Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COVID-19: Maandalizi ya kuelekea “kawaida mpya” katika makao makuu ya UN

Mfanyakazi wa usafi akideki kwa kutumia gari maalum kwenye ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN /Manuel Elias
Mfanyakazi wa usafi akideki kwa kutumia gari maalum kwenye ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

COVID-19: Maandalizi ya kuelekea “kawaida mpya” katika makao makuu ya UN

Masuala ya UM

"Usalama na afya ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, wawakilishi wa nchi wanachama na wale wote ambao wanatumia jengo letu, ni kipaumbele cha kwanza. Kurejea kwa wafanyakazi jengoni kutazingatia mapendekezo ya jiji na jimbo la New York, ambayo watafuata kadri yatakavyokuja.” Atul Khare, Msaidizi wa Katibu Mkuu katika Operesheni.
 

Baada ya kurejea katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kufuatia miezi kadhaa ya kufanyia kazi nyumbani kutokana na janga la COVID-19, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, wanadiplomasia, wawakilishi wa mashirika ya kiraia na waandishi wa habari wanaoandikia habari zao kutoka eneo hilo, watalazimika kuzingatia kanuni mpya zilizoandaliwa: mwelekeo wa upande mmoja kwa waendao kwa miguu, lifti kutobeba zaidi ya watu wawili, kuvaa barakoa, na kuketi angalau umbali wa mita 2 kutoka mtu mwingine.

Wafanyakazi wakiweka alama katika ushoroba wa wageni ulioko katika jengo la ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ili kuhakikisha kuwa waendao wa miguu wanafuata mwelekeo wa upande mmoja na hivyo kuwezesha kudhibiti umbali wa watu kutosogeleana.
UN Photo/Manuel Elías
Wafanyakazi wakiweka alama katika ushoroba wa wageni ulioko katika jengo la ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ili kuhakikisha kuwa waendao wa miguu wanafuata mwelekeo wa upande mmoja na hivyo kuwezesha kudhibiti umbali wa watu kutosogeleana.

Kwa kuzingatia wa miongozo ya afya ya mamlaka za jiji la New York, makao makuu ya Umoja wa Mataifa bado yamefungwa kwa umma tangu katikati ya mwezi Machi mwaka huu, ni wafanyazi wachache wapatao 100 ndio wanakwenda kazini kwa kuwa wanahitajika kuwepo jengoni. Kadri jiji la New York litakavyolegeza masharti ,vivyo hivyo UN nayo inajiandaa kurejea katika hali ya kawaida, na kurejea huko kutafanyika kwa awamu tatu.

Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiweka alama kwenye jengo eneo la kupokea wageni la jengo la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
UN /Manuel Elias
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiweka alama kwenye jengo eneo la kupokea wageni la jengo la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

"Usalama na afya ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, wawakilishi wa nchi wanachama na wale wote ambao wanatumia jengo letu, ni kipaumbele cha kwanza. Kurejea kwa wafanyakazi jengoni kutazingatia mapendekezo ya jiji na jimbo la New York, ambayo watafuata kadri yatakavyokuja.” Atul Khare, Msaidizi wa Katibu Mkuu katika Operesheni.

Kwa mujibu wa Idara ya Operesheni na Usaidizi, DOS, mfumo wa kurejea uko katika hatua za mwisho ambapo itaanza awamu ya kwanza. Wafanyakazi wanaohusika na huduma za ufungaji wa mitambo na biashara, FCAS, wanafanya kazi kuandaa ofisi na vyumba vya mikutano.

Usafi wa vifaa ukifanyika kwa dhati kwenye ofisi za jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa.
UN Photo/Manuel Elías
Usafi wa vifaa ukifanyika kwa dhati kwenye ofisi za jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa.

Tayari kuna vikundi vinafanya kazi kusafisha kwa kutumia dawa za kuuua vidudu maeneo ambayo yako hatarini zaidi na kuna miguso mingi kwenye jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Ikiwemo jengo lenye ghorofa 39 ambalo ni la sekretarieti, ukumbi wa Baraza Ku una majengo ya vyumba vya mikutano na maktaba.

Wafanyakazi hao wanasafisha kwa kina kila wakati maeneo ambayo yanatumika mara kwa mara ikiwemo shoroba, liftin a vyombo bila kusahau samani, vitasa vya milango, swichi za taa, na ngazi.

Usafi wa kina ndani ya vyumba vya mikutano.
UN /Manuel Elias
Usafi wa kina ndani ya vyumba vya mikutano.


Wafanyakazi wa DOS wakiweka alama kwenye shoroba na kuta kuonyesha mwelekeo wa watembeo ndani ya jengo ili kuhakikisha iwapo kuna foleni, basi watu wanazingatia umbali wa mita mbili. Vituo vya kutakasa mikono pia vimewekwa kwenye kumbi na maeneo mengine yenye watu wengi, na angalau kituo kimoja cha kutakasa mikono katika kila ghorofa ya ofisi.

Awamu ya  1

Wakati wa awamu ya 1, ni shughuli chache tu zitaruhusiwa. Kwa ujumla jengo halitatakiwa kuwa na watu zaidi ya 400 kwa siku ikilinganishwa na watu 4,200 katika siku za kawaida kabla ya COVID-19. Kwa majengo ya ziada kama vile, DC1 na DC2, idadi ya watu kwa wakati mmoja inatakiwa iwe asilimia 10 ya kiwango cha siku za awali. Lengo ni kuwa na watu wanaotakiwa kuwepo ofisini ili waweze kufanya kazi zao. Shughuli nyingi zitaendelea kufanywa kutokea majumbani.

Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa akiwa amevaa barakoa na nyuma ni mabango ya maelezo ya jinsi ya kuepusha maambukizi ya virusi vya Corona.
UN /Manuel Elias
Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa akiwa amevaa barakoa na nyuma ni mabango ya maelezo ya jinsi ya kuepusha maambukizi ya virusi vya Corona.

Wafanyakazi ambao ni lazima wafikie jengoni, ni lazima wavae barakoa lakini hakutakuwepo na ulazima wa kupima joto la mwili ili kuingia jengoni. Vivyo hivyo uchunguzi wa COVDI-19 hautakuwa wa lazima kabla ya kurejea jengoni. Hata hivyo wafanyakazi ambao wanataka kupima virusi vya Corona, wanaweza kuwasiliana na Idara ya Afya na Usalama kazini, DHMOSH, kupitia kurasa maalum. Idara hii inaweza pia kufika nyumbani kwa mfanyakazi ili kupima virusi.

Watu wote ambao watakuwepo jengo la makao makuu, watalazimika kuvaa barakoa pindi wanapita maeneo yenye watu wengi kama vile kumbi, lifti, shoroba, vyooni na njia za kupita watembeao kwa miguu. Hata hivyo, hawatalazimika kuvaa barakoa pindi wanapokuwa kwenye ofisi zao.
Wakati wa awamu ya 1 na 2 ya kurejea, mikutano ya uso kwa uso, iwe ya kiutawala au ya shirika haitaruhusiwa.
Kuanza awamu ya 1, ni lazima amri iliyotangazwa na New York, ilegezwe..

Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa akipimwa ili kubaini iwapo aliambukizwa virusi vya Corona. Hapa ni katika kituo cha huduma ya afya kilichomo ndani ya jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.
Photo: UN Medical Service
Mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa akipimwa ili kubaini iwapo aliambukizwa virusi vya Corona. Hapa ni katika kituo cha huduma ya afya kilichomo ndani ya jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa, New York.

Awamu ya 2

Wakati wa awamu ya 2, idadi ya watu kwenye jengo la makao makuu litaongezwa taratibu hadi kuwa 1,100 kwa siku, sawa na asilimia 40 hadi 50 ya viwango vya kabla ya COVID-19. Wafanyakazi wengine wataendelea kufanyika kazi nyumbani. Kutoka awamu 1 kwenda ya 2, kutahitaji kupungua zaidi kwa maambukizi na kuimarishwa kwa mifumo ya afya ya jiji mwenyeji.

Stika hizi zinatengenezwa na zina maelezo ya umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu.
UN /Manuel Elias
Stika hizi zinatengenezwa na zina maelezo ya umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu.

 

Awamu ya 3 - "Kawaida mpya"

Stika hizi nyekundu zenye maelezo kuhusu umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu, zinabandikwa kwenye madawati kuonyesha kuwa hapo hapapaswi kuwepo mtu.
UN /Manuel Elias
Stika hizi nyekundu zenye maelezo kuhusu umbali unaotakiwa kati ya mtu na mtu, zinabandikwa kwenye madawati kuonyesha kuwa hapo hapapaswi kuwepo mtu.

Kipindi cha mpito kuelekea awamu ya 3 – kikijulikana kama “ukawaida mpya” – kitafanyika pindi hatari za maambukizi kazini zitakapokuwa zimepunguzwa kutoka kipindi cha kabla ya janga kuanza na vikwazo kuhusiana na COVID-19 viwe vimeondolewa na jiji na jimbo la New York., hususan vile vinavyohusu malezi ya watoto na shule za umma. DOS inazingatia kuwa bado ni mapema sana kuainisha kanuni za kazi wakati wa awamu hii ya 3.

Fundi kutoka Idara ya usaidizi Umoja wa Mataifa akishona barakoa kwa ajili ya matumizi ya wafanyakazi muhimu ambao sasa wanatakiwa kwenda ofisini.
UN /Manuel Elias
Fundi kutoka Idara ya usaidizi Umoja wa Mataifa akishona barakoa kwa ajili ya matumizi ya wafanyakazi muhimu ambao sasa wanatakiwa kwenda ofisini.

Mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa

Muundo wa mjadala mkuu wa mwaka wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, uliopangwa kufanyika mwezi Septemba, kwenye makao makuu wakati wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu, sambamba na mikutano mingine ya ngazi ya juu, unaweza kubadilika.

Katika barua yake kwa Rais wa Baraza Kuu, Tijjani Muhammad-Bande, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, alipendekeza kuwa Baraza Kuu lifanye mjadala wake kwa mfumo tofauti. Mathalani, linaweza kutumia ujumbe uliorekodiwa awali kutoka kwa wakuu wa nchi na serikali au mawaziri, na kupunguza idadi ya watu watakaokuwepo kwenye ukumbi wa Baraza Kuu kuwa mwakilishi mmoja kwa kila ubalozi wenye makao yake New York.

"COVID-19 imebadili jinsi tunavyoishi na tunavyoshirikiana,” amesema msaidizi wa Katibu Mkuu, Atul Khare, akiongeza kuwa,  “lakini tuna mnepo na pamoja tunaweza kushinda hili, huku tukiheshimu, bila shaka umbali wa kutogusana.”

Mfanyakazi kutoka Idara ya usaidizi Umoja wa Mataifa akipanga barakoa kwa ajili ya matumizi ya wafanyakazi muhimu ambao sasa wanatakiwa kwenda ofisini.
UN /Manuel Elias
Mfanyakazi kutoka Idara ya usaidizi Umoja wa Mataifa akipanga barakoa kwa ajili ya matumizi ya wafanyakazi muhimu ambao sasa wanatakiwa kwenda ofisini.

Taarifa kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa: kadri janga linavyozidi kubadilika wiki zijazo, taarifa kuhusu mpango wa kurejea awamu ya 3 zitakuwa zinaongezwa kwenye ukurasa wa “afya na usalama wa kitengo cha menejimenti ya majanga na kuchapishwa kwenye Pahala Petu pa Kazi,  wavuti ya Iseek.