Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Lang Lang, Celine Dion, Lady Gaga na Andrea Bocelli pwakitumbuiza katika tamasha la One World, together at Home la UN

Kwa pamoja tutalishinda janga la COVID-19:Guterres

Picha kutoka kwenye Video
Lang Lang, Celine Dion, Lady Gaga na Andrea Bocelli pwakitumbuiza katika tamasha la One World, together at Home la UN

Kwa pamoja tutalishinda janga la COVID-19:Guterres

Afya

Tunakabiliana na tatizo lisilo na mithili yake. Ili kulishinda, ni sharti tuungane. Tatizo hili ni mliko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 

 

 

 

Tunakabiliana na tatizo lisilo na mithili yake. Ili kulishinda, ni sharti tuungane.

Hiyo ni kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe maalum alioutuma kwenye tamasha maalum la kimataifa la muziki liitwalo “One World Together at Home” au Dunia moja , pamoja nyumbani lililofanyika leo Jumamosi likijumuisha wanamuzikia mbalimbali, wahisani na wadau mbalimbali na wasanii.

Guterres amesema “Leo, kupitia muziki, ambao ni lugha ya wote, tunapongeza ujasiri na kujitolea kwa mashujaa wa afya na wengineo. Tunapofanya hivyo, hebu na tuwakumbuke walio hatarini zaidi.”

Mkusanyiko wa picha kutoka kwenye tamasha la One worl lililoandaiwa na Umoja wa Mataifa kusaidia wahudumu wa afya kote duniani kupambana na COVID-19
Picha kutoka kwenye Video
Mkusanyiko wa picha kutoka kwenye tamasha la One worl lililoandaiwa na Umoja wa Mataifa kusaidia wahudumu wa afya kote duniani kupambana na COVID-19

 

Amemtaka kila mmoja kujiunga kwenye wito wa usitishwaji mapigano kote duniani ili kujikita na adui yetu sote ambaye ni Virusi.

 

Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amewashukuru wote kwa kuunga mkono kazi ya kuokoa maisha ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO na mashirika mengine ya kibinadamu.

 

Amesisitiza kwamba “Pamoja, tutavishinda virusi hivi na kuujenga ulimwengu wenye usawa zaidi kama raia wa ulimwengu walioungana na mataifa yaliyoungana.”

Penye nia pana njia

Naye Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus akizungumza kuhusu tamasha hilo amesema penye nia pana njia na kwa pamoja hakuna linaloshindikana , akimuhimiza kila mtu, serikali, wahisani na wadau wote kushikamana ili kukabiliana na adui huyu wa kimataifa COVID-19.