Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Mtoto akiwa amebebwa na mamamke katika kituo cha afya nchini Mali.
UNICEF/UN0186355/Njiokiktjien

Watu bilioni 5 wakitarajiwa kukosa huduma za afya, UN kufanya mkutano wa kuchagiza huduma kwa wote

Watu bilioni 5 duniani wako hatarini kukosa huduma za afya ifikapo mwaka 2030 endapo nchi hazitochukua hatua kuziba mapengo ya upatikanaji wa huduma za afya imesema ripoti mpya iliyotolewa leo Jumapili, wakati Umoja wa Mataifa ukijiandaa kufanya mkutano wa kihistoria ili kuchagiza mchakato wa haraka kuhusu huduma za afya kwa wote.

Nickolay Mladenov, Mratibu Maalum wa mchakato wa amani Mashariki ya Kati  akihutubia Baraza la Usalama la UN
UN /Loey Felipe

Vitendo vya uchokozi vinahatarisha usalama Mashariki ya Kati:Mladenov

Wakati uhasama kati ya Israeli na Palestina ukiendelea kushuhudiwa, Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye mchakato wa amani huko Mashariki ya Kati Nickolay Mladenov ameelezea kuhusu hali mbaya inayoendelea ambako vitendo vya kigaidi, mashambulizi dhidi ya raia, makabiliano na waandamanji, uharibifu wa mali, kujengwa kwa makazi ya walowezi na janga la ufadhili ambavyo vimesababisha hali iliyokuwa mbaya kudorora zaidi.