Miji kote ulimwenguni ni ‘sababu kuu ya mabadiliko tabianchi’- UN-Habitat
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la makazi la Umoja wa Mataifa UN-Habitat Maimunah Mohd Sharif, miji kote ulimwenguni ni ‘sababu kuu ya mabadiliko tabianchi’ ingawa pia inaweza kuwa na suluhisho la kupunguza hewa chafuzi gesi, ambazo zinasababisha joto ulimwenguni kuongezeka.