Vitendo vya uchokozi vinahatarisha usalama Mashariki ya Kati:Mladenov
Wakati uhasama kati ya Israeli na Palestina ukiendelea kushuhudiwa, Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye mchakato wa amani huko Mashariki ya Kati Nickolay Mladenov ameelezea kuhusu hali mbaya inayoendelea ambako vitendo vya kigaidi, mashambulizi dhidi ya raia, makabiliano na waandamanji, uharibifu wa mali, kujengwa kwa makazi ya walowezi na janga la ufadhili ambavyo vimesababisha hali iliyokuwa mbaya kudorora zaidi.