Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

TANBAT 6

Mwambata wa jeshi wa Tanzania nchini atembelea Kikosi cha Tanzania TANBAT 6 wanaohudumu chini ya MINUSCA nchini CAR.

Mwambata jeshi wa Tanzania anayehudumu kazi yake Jamhuri ya Afrika ya kati Brigedia Jenerali Absolomon Lyanga Shausi amefanya ziara ya kutembelea kikosi cha walinda amani wa Tanzania TANBAT6 wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati MINUSCA ili kujitambilisha tangu kikosi hicho kianze shughuli ya ulinzi wa amani kikipokea majukumu kutoka kwa kikosi cha TANBAT5 mwishoni mwa mwaka.

Kapteni Mwijage Inyoma aliyeko nchini Afrika ya Kati anaeleza zaidi..

Audio Duration
2'31"
UN News

Jukwaa la vijana limetukutanisha na watunga sera za mataifa mbalimbali

Tayari tangu jana Aprili 25, Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) la mwaka 2023 limeng’oa nanga ambapo maelfu ya viongozi vijana kutoka duniani kote wanakusanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York kujadili pamoja na mambo mengine, masuala yanayolenga kuharakisha kujikwamua kutoka janga la COVID-19 na utekelezaji kamili wa Ajenda ya 2030 ya Malengo ya Maendeleo Endelevu. 

Sauti
3'39"
UNMISS

Wananchi wa Sudan Kusini washerehekea tamasha la utamaduni la amani

Mwanzoni mwa mwezi huu wa April dunia iliadhimisha Siku ya Kimataifa ya michezo kwa maendeo na amani, nchini Sudan Kusini kwa siku mbili mfululizo maelfu ya wananchi walikusanyika kusherehekea tamasha la utamaduni la amani lililoandaliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni ya jimbo la Kaskazini la Bahr El Ghazal.

Maelfu ya wananchi walikusanyika kwa ajili ya sherehe hizo katika mji wa Aweil, wakitazama na kushiriki kuimba na kucheza nyimbo na ngoma za kitamaduni. Leah Mushi anasimulia hali ilivyokuwa

Sauti
4'27"
UN News/Florence Westergard

Nguo hizi za binti yangu ni ushahidi tosha kuwa mauaji ya kimbari yapo: Manusura mauaji ya Rwanda

Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika maonesho yaliyopatiwa jina Simulizi za Manusura na Kumbukizi: Wito wa kuchukua hatua kuzuia mauaji ya kimbari. Katika maonesho haya vifaa mbali mbali vinavyohusiana na mauaji ya kimbari, mathalani ya Rwanda au kule Bosnia Hezergovina na Srebenica vinaoneshwa, yakiwemo mavazi ya wale waliokumbwa na mauaji hayo. Mauaji ya kimbari nchini Rwanda yalifanyika kwa siku 100 kuanzia Aprili 7 hadi Julai 15 mwaka 1994. Hadi leo hii manusura na wale waliopoteza ndugu na jamaa zao bado machungu yako moyoni mwao na wanatumia maonesho haya kupata sauti.

Sauti
4'39"
UN News

Athari za utupaji wa taka za plastiki kwenye maziwa na baharí

Uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya bahari unatajwa kuwa na athari kwa viumbe hai waishio chini ya maji kutokana na baadhi ya taka ikiwemo plastiki kuwa na madhara ya moja kwa moja kwa viumbe hao.

Umoja wa Mataifa umekuwa ukizitaka nchi wanachama kuhakikisha wanadhibiti taka hizo katika mataifa yao ili kuokoa Maisha ya viumbe hai waishio chini ya maji pamoja na mfumo wa Ikolojia.

Sauti
3'5"
Chadron's Hope Foundation/Elly Kitally

Nimejifunza watu wenye Down Syndrome wanaweza kuishi maisha ya kawaida wakijumuishwa – Elly Kitaly

Hivi karibuni katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa umefanyika mkutano wa Siku ya Kimataifa ya Down Syndrome. Mkutano huo uliokuwa na kauli mbiu “Pamoja nasi, kwa ajili yetu” uliandaliwa na taasisi ya Down Syndrome International (DSI) kwa kushirikiana na taasisi ya The International Disability Alliance (IDA), Uwakilishi wa kudumu katika Umoja wa Mataifa wa Brazil, Japan na Poland.  

Sauti
3'14"