Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nguo hizi za binti yangu ni ushahidi tosha kuwa mauaji ya kimbari yapo: Manusura mauaji ya Rwanda

Nguo hizi za binti yangu ni ushahidi tosha kuwa mauaji ya kimbari yapo: Manusura mauaji ya Rwanda

Pakua

Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika maonesho yaliyopatiwa jina Simulizi za Manusura na Kumbukizi: Wito wa kuchukua hatua kuzuia mauaji ya kimbari. Katika maonesho haya vifaa mbali mbali vinavyohusiana na mauaji ya kimbari, mathalani ya Rwanda au kule Bosnia Hezergovina na Srebenica vinaoneshwa, yakiwemo mavazi ya wale waliokumbwa na mauaji hayo. Mauaji ya kimbari nchini Rwanda yalifanyika kwa siku 100 kuanzia Aprili 7 hadi Julai 15 mwaka 1994. Hadi leo hii manusura na wale waliopoteza ndugu na jamaa zao bado machungu yako moyoni mwao na wanatumia maonesho haya kupata sauti. Hicho ndio msingi wa makala hii kama ilivyoandaliwa na kusimuliwa na Assumpta Massoi. 

Audio Credit
Sarah Oleng/Assumpta Massoi
Audio Duration
4'39"
Photo Credit
UN News/Florence Westergard