Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wananchi wa Sudan Kusini washerehekea tamasha la utamaduni la amani

Wananchi wa Sudan Kusini washerehekea tamasha la utamaduni la amani

Pakua

Mwanzoni mwa mwezi huu wa April dunia iliadhimisha Siku ya Kimataifa ya michezo kwa maendeo na amani, nchini Sudan Kusini kwa siku mbili mfululizo maelfu ya wananchi walikusanyika kusherehekea tamasha la utamaduni la amani lililoandaliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni ya jimbo la Kaskazini la Bahr El Ghazal.

Maelfu ya wananchi walikusanyika kwa ajili ya sherehe hizo katika mji wa Aweil, wakitazama na kushiriki kuimba na kucheza nyimbo na ngoma za kitamaduni. Leah Mushi anasimulia hali ilivyokuwa

Audio Credit
Selina Jerobon/Leah Mushi
Audio Duration
4'27"
Photo Credit
UNMISS