Simulizi ya Binti Armen Gakani, Mkimbizi Kalobeyei
Migogoro ya miongo na miongo nchini Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo, DRC imefurusha watu wengi kutoka makazi yao, wengine kubaki wakimbizi wa ndani na wengnine kukimbilia nchi Jirani. Kenya ni mojawapo wa nchi ambazo zinawahifadhi wakimbizi hao na katika Kaunti ya Turkana, tunakutana na Armen Gakani, msichana mwenye umri wa miaka 23 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ambaye alikimbia machafuko nchini humo na sasa yeye, akiwa na mama yake na wadogo wake wawili wenye ulemavu wanaishi katika kambi ya wakimbizi ya Kalibeyei. Je, ni kwa jinsi gani wameweza kujimudu kimaisha?