Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN/George Musubao

Msaada kutoka TANZBATT 10 umenusuru wagonjwa wanaokabiliwa na njaa

Mgeni njoo mwenyeji apone ni methali iliyodhihirisha huko eneo la Mbau jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC baada ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania kikosi cha 10, TANZBATT 10 walipotembelea hospitali ya La Grace kutoa msaada si tu wa chakula bali pia dawa. Walinda amani hawa wanahudumu kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO.

Sauti
4'
© UNICEF/Juan Haro

Wakati wa mafuriko nilipoteza mtoto, na sasa sina uhakika nitakayejifungua ataishi- Mkazi Pakistani

Mwaka mmoja tangu mafuriko ya kihistoria yakumbe Pakistani, na hali ya dharura nchini humo kutangazwa, mamilioni ya watoto bado wanaendelea kuhitaji misaada ya dharura huku operesheni za ukarabati zikisalia kukumbwa na ukata kwani fedha zinazotakiwa hazijapatikana. Hii leo katika Makala Assumpta Massoi anakupeleka Pakistani kusikia waathirika na kumbukumbu za hali ilivyokuwa, shaka na shuku zao hivi sasa na nini Umoja wa Mataifa unafanya kuleta angalau ahueni. 

Sauti
4'23"
© WHO/Michael Duff

Mifumo madhubuti ya kuwasiliana Sierra Leone imeimarisha uthibiti wa milipuko ya magonjwa

Takriban miaka 10 iliyopita nchi kadhaa za Afrika zilikumbana na mlipuko wa ugonjwa hatari wa ebola uliogharimu maisha ya mamilioni ya watu. Moja ya nchi hizo ni Sierra Leone ambayo wakati mlipuko wa Ebola ukiikumba nchi hiyo walikuwa hawana njia bora za kuwasiliana kama taifa na kujua ukubwa wa ugonjwa huo na namna ya kudhibiti. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika mbali na kuisaidia nchi hiyo kupamba na Ebola lakini iliwasaidia kuweka mifumo madhubuti ya kuwasiliana nchi nzima kujua iwapo kuna mlipuko wa ugonjwa wowote.

Sauti
4'30"
© UNOCHA/Yao Chen

Wahisani msichoke kukirimu wenye uhitaji – Gregory Akall wa OCHA

Siku ya watoa misaada ya kibinadamu huadhimishwa kila Agosti 19, na maudhui mwaka huu ni “kwa vyovyote vile,” ikimaanisha misaada lazima iendelewe kutolewa katika mazingira yoyote yale. Gregory Akall wa Ofisa wa usaidizi wa kibinadamu katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya misaada ya binadamu na ya dharura (OCHA), anahudumu kaskazini mwa Kenya.

Sauti
4'4"
© UNOCHA/M. Minasi

Sikufahamu jinsi ya kuzungumza na mwanangu kumuepusha na mimba za utotoni - Mzazi Haiti

Hebu fikiria kutarajia kupata mtoto wakati ambapo hata hufahamu neno ujauzito lina maana gani. Hicho ndicho kilichomfika mtoto mwenye umri wa miaka 14 nchini Haiti ambaye alijikuta anapewa ujauzito na kaka wa rafiki ya kiume wa rafiki yake. Hakuwa anajitambua akakubali kumsindikiza rafiki yake na zaidi ya yote akakubali urafiki na kijana huyo mwenye umri wa miaka 16. Mama yake binti huyu naye anasema hakufahamu ni kwa jinsi gani azungumze na mtoto wake ili kumuepusha na uhusiano na wavulana kwa lengo la kumuepusha kupata ujauzito.

Sauti
4'17"
UNISFA

Kamishna Susan aelezea ambacho hatosahau wakati wa huduma yake Abyei

Hii leo katika makala nakukutanisha na Kamishna Susan Kaganda, Mkuu huyu wa Utawala na Raslimali watu katika Jeshi la Polisi Tanzania ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa  Operesheni kwenye ujumbe wa muda wa Umoja wa Mataifa wa mpito kwenye eneo la Abyei lililoko katikati ya Sudan na Sudan Kusini, UNISFA. Katika mahojiano yake na Stella Vuzo wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC Dar es salaam nchini Tanzania anasimulia mambo kadhaa ikiwemo hili analoanza nalo la jambo gani anakumbuka zaidi wakati akihudumu UNISFA. 

Sauti
4'59"
© Virginia Sintanai and Bernard Loolasho/KIYN-LANCCI

Vijana wa jamii ya asili tuna nafasi kubwa kusongesha jamii zetu

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya jamii ya watu wa asili hii leo, ambayo maudhui yake yanalenga vijana na nafasi yao katika kusongesha tamaduni na ufahamu wa jamii hizo Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ilibisha hodi nchini Kenya, Mashariki mwa Afrika ambako kuna vijana wa jamii ya asili wanachukua hatua. Lengo ni kufahamu nafasi yao hivi sasa na nini wanafanya kuona mustakabali wao unaimarika. Vijana hao Virginia Sintanai wa jamii ya Ilchamus na pia mwanachama wa Mtandao wa vijana wa jamii ya asili nchini Kenya (KIYN).

Sauti
4'21"
UN News/Thelmaa Mwadzaya

Watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama wana afya bora - UNICEF Kenya

Wiki ya unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama duniani, imehitimishwa Agosti 7, au jana Jumatatu, wiki iliyosheheni matukio ya kuonesha hatua za kuhakikisha watoto wanapozaliwa wananyonyeshwa maziwa ya mama kwa faida sio tu ya mtoto bali pia mama. Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na Wizara ya Afya, walikuwa na tukio la aina hiyo na shuhuda wetu alikuwa mwandishi wetu nchini Kenya, Thelma Mwadzaya.

Sauti
6'58"
© Unsplash/Possessed Photograph

Mauritius waelekeza mbinu wanazotumia kutokomeza uvutaji wa tumbaku nchini mwao

Mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Afya WHO walitoa ripoti ya 9 kuhusu janga la uvutaji tumbaku na kueleza kuwa mafanikio yameanza kuonekana kwa nchi wanachama kutekeleza sera ya kulinda umma kutoathirika na uvutaji wa sigara unaofanywa na mtu mwingine ambapo zaidi ya watu bilioni 5.6 wamenufaika na sera hiyo ulimwenguni kote. Nchi ya Mauritius ilipongezwa kwa kuwa nchi pekee iliyotekeleza vyema sera zote sita za kupambana na athari za tumbaku. Je waliwezaje?

Sauti
3'54"
UN Brazil

Amina J. Mohammed ziarani Amazon: Nimesikia maombi yenu na tutapaza sauti

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed anaendele ana ziara yake ya siku tano nchini Brazil ambapo siku ya Alhamisi Agosti 3, 2023 alizuru jamii ya watu wa asili ya Mapuera kwenye ukanda wa Amazon jimboni Para ambako huko alipata fursa ya kuzungumza na wanajamii hao na kusikia maombi yao, ziara ambayo anafanya kufuatilia utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuelekea mkutano wa viongozi kuhusu SDGs mwezi Septemba mwaka huu. Thelma Mwadzaya anatusimulia kilichojiri. 

Sauti
3'46"