Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNDP Zimbabwe

Je unafahamu kuwa kuna fursa ya ufadhili katika nishati safi na salama Tanzania?

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la mfuko wa maendeleo ya mitaji UNCDF wakizingatia Utafiti wa Bajeti ya Kaya Tanzania Bara (2017/18), upatikanaji wa nishati safi na teknolojia ya kupikia ni asilimia 17.1 tu ya wakazi wa mijini na asilimia 2 ya wakazi wa vijijini. Kuongezeka kwa mahitaji ya nishati ya kuni kunatokana na ukuaji wa haraka wa miji, bei ya juu, na upatikanaji mdogo wa nishati mbadala.

Sauti
5'22"
Credit: UN/Assumpta Massoi

Kutoka Dodoma Tanzania Bara hadi Paje, Zanzibar kukabiliana na  umaskini

Moja ya malengo ya Umoja wa Mataifa kuhusu maendeleo endelevu, SDGs ni kutokomeza umaskini ifikapo mwaka 2030. Ikiwa imesalia miaka 7 kabla ya kufikia ukomo, nchi, jamii na kila mtu mmoja mmoja anachukua hatua kutokomeza umaskini hasa kuanzia ngazi ya familia. Umaskini unasababisha watu washindwe sio tu kupata mlo bali pia kupeleka watoto wao shuleni kupata elimu bora.

Sauti
3'36"
UNHCR Video

Kutana na Timu ya Taifa ya Kandanda ya Wanawake ya Afghanistan - Wakimbizi katika Michezo

“Tunajaribu kuleta michezo na nguvu zake katika mazingira magumu sana ya watu wasiojiweza. Mchezo ni mzuri kwa kuwapa watu matumaini ya siku zijazo.” Anasema Filippo Grandi, Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) akirejelea Timu ya mpira wa miguu ya wanawake wakimbizi wanaoishi nchini Australia baada ya kuokoa maisha yao yaliyokuwa hatarini nchini mwao Afghanistan. Anold Kayanda anasimulia zaidi. 

Sauti
4'17"
UN/Eugene Uwimana

WD2023 imeonesha kuwa wanawake tunachukua hatua mashinani - Martha Wanza

Mkutano wa kimataifa wa Women Deliver 2023 (WD2023) au wanawake wanatekeleza umekunja jamvi mwishoni mwa wiki mjini Kigali nchini Rwanda baada ya kuwaleta pamoja washiriki 6,000 ana kwa ana na wengine zaidi ya 200,000 mtandaoni. Lengo kuu la mkutano huo mkubwa kabisa uliozanza Julai 17 hadi 20 na kubeba kaulimbiu “Nafasi, mshikamano na suluhu” lilijikita katika ujumuishwaji ili kusongesha usawa endelevu wa kijinsia kwa kuhusisha sekta mbalimbali.

Sauti
4'8"
UN News/George Musubao

Asante UNMAS kwa kutegua bomu lililotishia uhai wetu- Wananchi Kididiwe, DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo - DRC, Shirika la Umoja wa Mataifa la kutegua Mabomu ya ardhini (UNMAS) Jumanne Julai 18 mwaka huu wa 2023  lilitegua bomu lenye uzito wa kilo 250 lililogunduliwa wiki iliyopita na wakulima katika eneo la Kididiwe, wilayani Beni. Jimboni Kivu Kaskazini. Wakazi wanaonesha furaha yao kwa Umoja wa Mataifa kwa kutegua bomu hilo linalosababisha vifo.  Mwandishi wetu wa nchini DRC, George Musubao amefuatilia na kuandaa makala hii. 

Sauti
3'55"
Stella Vuzo/UNIC Dar es

Sauti za asasi za kiraia katika utekelezaji wa SDGs ni muhimu: UNA

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa la Umoja wa Mataifa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu HLPF, linaendelea hapa Makao Makuu jijini New York Marekani likitathimini utekelezaji wa malengo hayo yaliyosaliza chini ya miaka 7, kabla ya kufikia ukomo hapo mwaka 2030. Mbali ya tathimini ya utekelezaji wake jukwaa hilo limetoa fursa kwa nchi 39 zilizojitolea kuwasilisha ripoti za kitaifa za utekelezaji wa malengo hayo. Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo na iliwasilisha ripoti yake jana Jumanne.

Sauti
3'52"
Pan American Health Organization

Kesho isiyo na saratani ya shingo ya kizazi kwa Wanawake Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni kanda ya Afrika linaeleza kuwa Saratani ya shingo ya kizazi ni moja ya sababu kuu za vifo vinavyotokana na saratani kwa wanawake nchini Tanzania. Kawaida saratani ya shingo ya kizazi huathiri wanawake wenye zaidi ya umri wa miaka 25 ambao wameambukizwa virusi vya papilloma ya binadamu na hawajapata chanjo. Makala hii iliyoandaliwa na WHO na kusimuliwa na Anold Kayanda inaeleza jinsi uchunguzi wa afya wa mara kwa mara ni njia nzuri ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi..  
 

Sauti
3'23"
UN Women/Luke Horswell

UNFPA Kenya yaeleza mipango yake ya kutetea haki za wanawake

Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Umoja wa Mataifa la afya ya uzazi na idadi ya watu UNFPA nchini Kenya Anders Tomsen, ameeleza shirika hilo linatekeleza ipasavyo tamko la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu ambalo mwaka huu linafikisha miaka 75 hususan ibara ya Tano ambayo inasema Haki ya mtu ya kwamba asitumbukizwe kwenye vitendo vya mateso, ukatili, au adhabu dhalili.

Akihojiwa na mwandishi wetu wa Kenya Thelma Mwadzaya Tomsen anaanza kwa kusema shirika hilo limeundwa kwa kuzingatia misingi ya haki. 

Sauti
3'2"